Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/12/07
“Katika kipindi cha sikukuu, watu wengi wanajaribu kuwa wema na wenye huruma. Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa mahali pazuri ikiwa watu wangeonyeshana huruma katika mwaka wote? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Petro 3:8.] Gazeti hili linazungumzia faida ya kuonyesha huruma na linaonyesha njia fulani ambazo katika hizo tunaweza kuonyesha huruma.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Je, unafikiri kwamba wapendwa wetu waliokufa wataishi tena? [Acha mtu ajibu.] Biblia inasema kwamba kuna njia ya kutoka katika kifo. [Soma Zaburi 68:20.] Gazeti hili linaonyesha kwa nini hatupaswi kuogopa kifo na kufikiri kwamba kifo ndio mwisho kabisa wa maisha.”
Mnara wa Mlinzi 01/01/08
“Watu wengi wanasali kwamba Ufalme wa Mungu uje. Kwa mfano, ona sala hii yenye kujulikana sana ambayo Yesu alifundisha wafuasi wake. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Je, umekwisha kujiuliza Ufalme wa Mungu ni nini na utakuja wakati gani? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo.”
Amkeni! Mwezi wa 1
“Katika historia yote wanawake wamesumbuliwa na ubaguzi na kutendewa vibaya. Unafikiri inakuwa hivyo sababu gani? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyoagiza waume kutendea wake zao. [Soma 1 Petro 3:7.] Gazeti hili linazungumzia mawazo ya Biblia yenye kuonyesha maoni ya Mungu na ya Kristo kuelekea wanawake.”