Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Watu wengi wanahangaishwa kuona jinsi majira ya sikukuu yamefanywa kuwa ya kibiashara. Je, unafikiri kwamba mazoea hayo yamekwenda kinyume na mradi wa sikukuu hizo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi desturi za sikukuu zimebadilika kadiri wakati unavyopita. Linazungumzia pia jinsi tunavyoweza kwa kweli kumheshimu Mungu na Kristo.” Soma Yohana 17:3.
Amkeni! Des. 22
“Miaka 85 hivi iliyopita, ugonjwa wenye kuenea haraka uliua watu wengi zaidi katika majuma 24 kuliko wale ambao UKIMWI umeua katika miaka 24. Wengine wanaita ugonjwa huo tauni mbaya zaidi katika historia. Je, umekwisha kusikia habari ya homa ya Kihispania (grippe espagnole)? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia ikiwa jambo la namna hiyo linaweza kutukia tena. Linatoa pia sababu ya kuwa na tumaini.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Watu wana uwezo wa kufanya mambo mengi mazuri, lakini mara nyingi wanafanya mambo maovu yasiyoweza kuelezwa. Je, umekwisha kujiuliza kwa nini hivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa jibu la Biblia. Linaeleza pia jinsi mema yatashinda uovu mwishowe.” Soma Waroma 16:20.
Amkeni! Jan.
“Je, umejiuliza wakati wowote namna gani ulimwengu utakavyokuwa mnamo miaka 20 au 30? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 119:105.] Biblia inatoa mwangaza hivi kwamba tunaweza kutambua yale ambayo wakati ujao unatuwekea. Gazeti hili linachunguza unabii mbalimbali unaoonyesha mahali tulipo sasa katika kipindi cha wakati na kwa nini tunaweza kutarajia wakati ujao mwangavu.”