Tufuate Mfano Ambao Yesu Alituwekea
1 Tunaposhiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi, tunapaswa kukumbuka kwamba mfano wetu unaweza kuchochea sana wale wanaotutazama. Yesu alifundisha kupitia maneno na matendo. Wale waliomtazama waliweza kuona bidii yake, upendo wake kwa watu, nia yake kubwa ya kutakasa jina la Baba yake, na kusudi lake la kutimiza mapenzi ya Baba yake.—1 Pet. 2:21.
2 Tunapohubiri Nyumba kwa Nyumba: Kama vile mfano wa Yesu ulivyochochea wengine, mfano wetu unachochea wale tunaotumika nao. Wahubiri wapya na wale wahubiri wasio na uzoefu mwingi wanapotuona tukijitoa kwa bidii katika kazi ya kuhubiri, watafikiri kuhusu jinsi wanavyoweza kufanya kazi yao ya kuhubiri iwe nzuri zaidi. Wanapoona furaha yetu na jinsi tunavyopendezwa na wengine, watakumbuka kwamba ni jambo la maana kuonyesha sifa hizo katika kazi yao ya kuhubiri. Wanapotambua bidii yetu katika kutumia Maandiko, katika kurudilia watu tuliohubiria, na katika kuongoza mafunzo ya Biblia, watachochewa kufanya vivyo hivyo.
3 Tunapoongoza Mafunzo ya Biblia: Watu tunaojifunza nao Biblia watatazama zaidi sana mwenendo wetu. Kwa mfano, hata ikiwa tunaweza kuwafasiria kwamba ni jambo la lazima kutayarisha funzo, kusoma maandiko, na kutia kistari chini ya mambo makuu, wataona ikiwa sisi pia tumejitayarisha. (Rom. 2:21) Ikiwa tunafika pa wakati ambao tulipanga kujifunza nao, hawataruhusu mambo mengine yawazuie kujifunza Biblia. Bila shaka, watatambua roho ya kujitoa tuliyo nayo katika kazi ya kuhubiri na imani yetu yenye nguvu. Haishangazi kwamba wale wanaojifunza na wahubiri wanaofuata kabisa mfano wa Yesu, mara nyingi wanakuwa wahubiri wenye bidii na wenye matokeo zaidi.
4 Tunapohuzuria Mikutano ya Kutaniko: Wale wote walio katika kutaniko la Kikristo wana daraka la kufundisha kupitia mfano katika mikutano ya kutaniko. Wale wenye kupendezwa wanaoanza kuhuzuria mikutano wanapata faida kutokana na mfano mwema wanaoona katika kutaniko. Watatambua kwamba washiriki wa kutaniko wana urafiki mchangamfu na umoja wa Kikristo, na wanavalia na kujipamba kwa kiasi. (Zab. 133:1) Watatambua pia mfano tunaoonyesha kwa kuhuzuria kwa uaminifu mikutano ya kutaniko na kutangaza imani yetu mbele ya watu wote. Mgeni mmoja aliyehuzuria mmoja wa mikutano yetu aliona jinsi binti mdogo aliweza kupata kwa uharaka katika Biblia yake andiko lililotajwa na jinsi alifuata usomaji kwa uangalifu. Mfano wa binti huyo ulimchochea kuomba funzo la Biblia.
5 Maandiko yanatutia moyo kufuata mfano mzuri wa wengine. (Flp. 3:17; Ebr. 13:7) Kwa hiyo, tunapaswa kukumbuka kwamba ikiwa tunafuata kabisa mfano ambao Yesu aliweka, wengine watatambua jambo hilo na wanaweza kuchochewa kwa njia nzuri. Tukijua hivyo, na tutie akilini maneno yanayopatikana katika andiko la 1 Timotheo 4:16: “Jiangalie daima wewe mwenyewe na kufundisha kwako.”
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni mfano gani ambao Yesu aliweka?
2. Ni katika njia gani mfano wetu unaweza kuchochea wale tunaohubiri nao?
3. Namna gani mfano wetu unaweza kufundisha wanafunzi wa Biblia, na wanaweza kujifunza nini?
4. Tunapohuzuria mikutano ya kutaniko, wengine wanajifunza nini kutokana na mfano wetu?
5. Kwa nini hatupaswi kupuuza hata kidogo umaana wa mfano wetu?