Fundisha Wapole Kutembea Katika Njia ya Mungu
1 Ilisemekana kwamba Wanafunzi wa Kristo wa karne ya kwanza walikuwa wa “Ile Njia.” (Mdo. 9:2) Ukristo wa kweli ni njia inayohusisha maisha yote ya mtu. (Met. 3:5, 6) Kwa hiyo, tunapoongoza mafunzo ya Biblia tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kumtolea tu mwanafunzi ujuzi sahihi wa mafundisho ya Biblia. Tunapaswa pia kusaidia wanafunzi wa Biblia kutembea katika njia ya Yehova.—Zab. 25:8, 9.
2 Kupenda Yehova na Yesu: Kwa kweli, ni vigumu kwa watu wasiokamilika kuambatanisha fikira zao, mitazamo, usemi, na mwenendo wao na mapenzi ya Mungu. (Rom. 7:21-23; Efe. 4:22-24) Hata hivyo, kumpenda Mungu na mwana wake kunachochea walio wapole wasishindwe na hali hizo. (Yoh. 14:15; 1 Yoh. 5:3) Tunawezaje kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wasitawishe upendo huo?
3 Saidia mwanafunzi wako apate kujua utu wa Yehova. Ndugu mmoja alieleza, “Watu hawawezi kumpenda mtu wasiyemjua, hivyo mwanzoni tu mwa funzo, mimi ninawafundisha jina la Mungu kutoka katika Biblia, nami ninatafuta nafasi za kukazia sifa za Yehova.” Kukazia mfano wa Yesu ni njia bora ya kufanya hivyo. (Yoh. 1:14; 14:9) Kwa kuongezea, fanya matumizi ya kisanduku cha kujikumbusha mwishoni mwa kila sura ya kitabu Biblia Inafundisha ili kusaidia mwanafunzi aonyeshe sifa nzuri ajabu za Mungu na Mwana wake.
4 Fundisha Kupitia Mfano Wako: Tukiwa walimu na viongozi, tunaonyesha wengine kupitia matendo yetu maana ya kutembea katika njia ya Mungu. (1 Kor. 11:1) Kwa mfano wanafunzi wengi wa Biblia hawazoei kuwakaribia watu wasiowajua ili kuwaelezea mambo wanayoamini. Kwa hiyo, huenda ikaomba uvumilivu na ufundi ili kuwasaidia wasitawishe upendo, imani, na ujasiri unaohitajiwa ili kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (2 Kor. 4:13; 1 The. 2:2) Tamaa yetu ya kuongoza wanafunzi wetu itatuchochea tuwe pamoja nao wanaposhiriki mara ya kwanza katika huduma ya Kikristo.
5 Mfano wako unaweza kufundisha wanafunzi katika sehemu zingine za maana zinazohusiana na maisha ya Kikristo. Unapotembelea wagonjwa au unaposalimu wengine kwa shauku kwenye mikutano ya kutaniko, wanaona uthibitisho wa upendo. (Yoh. 15:12) Unaposhiriki katika kusafisha Jumba la Ufalme na kufanya mambo ili kusaidia wengine, unawafunza jinsi ya kutumikia wengine. (Yoh. 13:12-15) Wanapoona kwamba una maisha yaliyo rahisi, wanaelewa maana ya ‘kutafuta kwanza ufalme.’—Mt. 6:33.
6 Kazi ya kufundisha wengine kutoka Neno la Mungu na kufanya wanafunzi inahusisha jitihada nyingi. Lakini ni furaha kabisa kuona wapole ‘wakiendelea kutembea katika kweli.’—3 Yoh. 4.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni nini linalohusika pia katika kufanya wanafunzi?
2. Ni nini kinachoweza kuchochea mwanafunzi wa Biblia kuzishika amri za Mungu?
3. Tunawezaje kusaidia wanafunzi wa Biblia kusitawisha upendo kwa Yehova na Yesu?
4. (a) Kwa nini wanafunzi wengi wanaona kuhubiri kuwa tatizo kubwa? (b) Tunawezaje kusaidia wanafunzi wetu wanaposhiriki mara ya kwanza katika huduma ya Kikristo?
5. Jinsi gani mfano mzuri unasaidia wanafunzi kujifunza mambo yanayohusika katika kufuata amri za Mungu?
6. Ni jambo gani linalotokana na kuwasaidia wapole wamtumikie Yehova?