Tuwafundishe Wengine Wampende Yehova
1 Je, unakumbuka wakati ulisikia kuhusu Yehova kwa mara ya kwanza? Ni jambo gani lililokuchochea umkaribie? Watu wengi walio na mioyo yenye haki watakuambia kwamba walimkaribia Muumba wetu walipojifunza kuhusu sifa zake nzuri sana, zaidi sana huruma na upendo wake.—1 Yoh. 4:8.
2 “Huyu Ndiye Mungu Wetu”: Kitabu Biblia inafundisha kinakazia upendo wa Yehova na uhitaji wa kufanya urafiki wa pekee pamoja naye. Namna gani tunaweza kutumia kitabu hicho ili kufundisha wengine wakomalishe upendo wao kwa Mungu? Tunapokazia wazo mpya, tunaweza kuuliza maulizo yanayosaidia watu wafikiri, kama vile: “Habari hii inafunua nini kuhusu Yehova?” ao “Ni katika njia gani habari hii inaonyesha kwamba Yehova ndiye Baba mzuri zaidi ambaye kila mutu angependa kuwa naye?” Kufundisha katika njia hii kunaweza kumsaidia mwanafunzi kuanza urafiki wenye kudumu pamoja na Yehova.
3 Tunaposaidia wanafunzi wa Biblia watambue kwamba ni pendeleo kubwa kupata ujuzi juu ya Mungu wa pekee wa kweli na aliye hai, watakubaliana na maneno haya ya Isaya: “huyu ndiye Mungu wetu.” (Isa. 25:9) Tunapofasiria neno la Mungu, tunapaswa kukazia jinsi wanadamu watakavyobarikiwa wakati makusudi ya Yehova yatakapotimia kupitia serikali ya Ufalme yenye kuongozwa na Kristo Yesu.—Isa. 9:6, 7.
4 Jinsi ya Kuonyesha Kwamba Tunampenda Yehova: Tunajua kwamba kumpenda Yehova kwa moyo wetu wote, nafsi yetu yote, na akili yetu yote kunahusisha mengi zaidi ya kujisikia wenye kuvutiwa naye sana. Tunapaswa kukubali na kushikamana na njia yake ya kufikiri. (Zab. 97:10) Tunaonyesha upendo wetu kwa Yehova kwa kutii amri zake zote na kuendelea katika “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu”.—2 Pet. 3:11; 2 Yoh. 6.
5 Kufanya mapenzi ya Mungu kwa sababu tunampenda kunaleta furaha. (Zab. 40:8) Mwanafunzi wa Biblia anapaswa kuelewa kwamba amri zote za Mungu zimetolewa kwa faida za milele za watumishi Wake. (Kum. 10:12, 13) Kwa kuishi kulingana na mwongozo wa Yehova, mutu anaonyesha kwamba anapendezwa sana na kazi Zake za ajabu. Saidia mwanafunzi aelewe kwamba kutembea katika njia za Yehova kutamulinda asipatwe na matatizo yenye kutokana na kuzarau njia za Mungu.
6 Baraka Wanazopata Wale Wanaompenda Mungu: Yehova anahangaikia sana watu wapole wanaompenda, na anawafunulia “mambo mazito ya Mungu.” (1 Kor. 2:9, 10) Kwa kujua makusudi ya Yehova, wanaelewa vizuri wakati ujao na wana tumaini hakika. (Yer. 29:11) Yehova anawaonyesha wema mwingi wale wanaompenda. (Kut. 20:6) Wanapendezwa na tumaini la uzima wa milele kwa sababu Mungu anawapenda sana.—Yoh. 3:16.
7 Kadiri tunavyopata kumjua Baba wetu wa mbinguni, ndivyo tunavyochochewa kuwaelezea wengine kumhusu. (Mt. 13:52) Ni pendeleo kubwa kabisa kufundisha wengine kumpenda Yehova, zaidi sana watoto wetu! (Kum. 6:5-7) Basi, sisi pamoja na wanafunzi wetu wa Biblia na tuendelee kumsifu Yehova tunapojionea ‘wingi wa wema wake.’—Zab. 145:7.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni nini kinachochochea watu fulani wamkaribie Yehova?
2, 3. Namna gani tunaweza kutumia kitabu Biblia Inafundisha ili kusaidia wanafunzi wa Biblia wakomalishe upendo wao kwa Yehova?
4, 5. Kumpenda Yehova kunamaanisha nini?
6. Mutu anaweza kupata baraka gani kwa sababu ya kumpenda Yehova?
7. Namna gani unaona kufundisha wengine kumpenda Yehova?