Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w20 Mwezi wa 3 uku. 2-7
  • Kumupenda Yehova na Kuwa Mwenye Shukrani Kutakuchochea Ubatizwe

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumupenda Yehova na Kuwa Mwenye Shukrani Kutakuchochea Ubatizwe
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUTU MWENYE TUNAPASWA KUPENDA ZAIDI
  • Juu ya Nini Unapaswa Kubatizwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Namna ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Ubatizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Ninapaswa Kutoa Maisha Yangu kwa Mungu na Kubatizwa?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • ‘Lazima Umupende Yehova Mungu Wako’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
w20 Mwezi wa 3 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 10

Kumupenda Yehova na Kuwa Mwenye Shukrani Kutakuchochea Ubatizwe

“Ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?”​—MDO. 8:36.

WIMBO 37 Kumtumikia Yehova kwa Nafsi Yote

KIFUPI CHA HABARIa

1-2. Kulingana na Matendo 8:27-31, 35-38, ni nini ilimuchochea ofisa Muetiopia abatizwe?

UNAPENDA kubatizwa ili ukuwe mwanafunzi wa Kristo? Kumupenda Yehova na kuwa wenye shukrani kwake kumechochea watu mingi wabatizwe. Fikiria mufano wa ofisa mwenye alikuwa anatumikia malkia wa Etiopia.

2 Ofisa Muetiopia alibatizwa kisha tu kujifunza katika Maandiko kama alipaswa kubatizwa. (Soma Matendo 8:27-31, 35-38.) Ni nini ilimuchochea? Ni wazi kwamba aliona Neno la Mungu kuwa la maana kwa sababu alikuwa anasoma maandiko fulani ya kitabu cha Isaya wakati alikuwa anasafiri mu gari kutoka Yerusalemu kuenda Etiopia. Na wakati Filipo alizungumuza naye, ule ofisa alionyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alikuwa amemufanyia. Lakini, sababu gani ule ofisa alisafiri kuenda Yerusalemu? Kwa sababu tayari alikuwa anamupenda Yehova. Ni nini inaonyesha vile? Alikuwa anatokea tu kumuabudu Yehova kule Yerusalemu. Inaonekana mwanamume huyu alikuwa ameacha dini ya wazazi wake na alikuwa amejiunga na taifa moja tu lenye lilikuwa limejitoa kwa Mungu wa kweli. Ni kumupenda Yehova njo kulimuchochea pia achukue hatua ingine ya maana: kubatizwa ili kuwa mwanafunzi wa Kristo.​—Mt. 28:19.

3. Ni nini inaweza kuzuia mutu asibatizwe? (Ona kisanduku “Moyo Wako Unafanana na Udongo wa Aina Gani?”)

3 Upendo kwa Yehova unaweza kukuchochea ubatizwe. Lakini upendo unaweza pia kukuzuia usibatizwe. Namna gani? Fikiria mifano fulani tu. Pengine unapenda sana watu wa familia yako na marafiki wako wenye hawako Mashahidi, na unaweza kuogopa kwamba watakuchukia kama unabatizwa. (Mt. 10:37) Ao pengine unapenda tabia zenye unajua kama Mungu anachukia, na unaweza kuona kama ni nguvu kuachana nazo. (Zb. 97:10) Ao pengine tangu wakati ulikuwa mutoto ulikuwa unafanya sikukuu zenye ziko na uhusiano na dini ya uongo. Pengine unaendelea kukumbuka mambo fulani ya muzuri juu ya sikukuu hizo. Kwa hiyo, unaweza kuona kama ni nguvu kuacha kufanya sikukuu zenye zinamuchukiza Yehova. (1 Ko. 10:20, 21) Njo maana ni muzuri ujiulize hivi: “Ni nini ao ni nani njo ninapenda zaidi?”

Moyo Wako Unafanana na Udongo wa Aina Gani?

Yesu alifananisha ujumbe wa Biblia na mbegu, na alifananisha mioyo ya wanadamu na aina mbalimbali za udongo. (Lu. 8:4-8) Pengine umejifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kwa wakati fulani. Inaweza kuwa muzuri usome Luka 8:11-15 na ujiulize hivi: ‘Moyo Wangu unafanana na udongo wa aina gani?’

  • Udongo wenye kukanyangwa-kanyangwa, na ndege iko anatafuta kutua juu yake.

    Udongo wenye kukanyangwa-kanyangwa: Huyu ni mutu mwenye hatumie wakati wa kutosha ili kutayarisha muzuri funzo lake la Biblia. Mara mingi anakosa kujifunza ao anakosa kuhuzuria mikutano juu iko na mambo mingi ya kufanya.

  • Udongo wenye miamba.

    Udongo wenye miamba: Huyu ni mutu mwenye anaacha mikazo na upinzani wa marafiki na wa watu wa familia yake vimuzuie kumutii Yehova na kuishi kulingana na kanuni zake.

  • Udongo wenye miiba.

    Udongo wenye miiba: Huyu ni mutu mwenye anapenda mambo yenye anajifunza juu ya Yehova, lakini anawaza kama kuwa na feza na vitu mingi njo kutamufanya akuwe na furaha na usalama. Mara mingi anakosa kujifunza juu iko anafanya kazi ao juu ya mambo ya kujifurahisha.

  • Udongo kwenye ngano inakomaa kwa uwingi.

    Udongo muzuri: Huyu ni mutu mwenye anajifunza Biblia kwa ukawaida na kutumikisha mambo yenye anajifunza. Jambo la maana sana mu maisha yake ni kumupendeza Yehova. Anaendelea kuambia wengine mambo yenye anajua juu ya Yehova hata kama anapambana na majaribu ao upinzani.

Ni wewe utaamua kama moyo wako utafanana na udongo wa aina gani. Kama vile aina mbalimbali za udongo wenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu, moyo wako wa mufano unaweza kuregezwa, kuondolewa majani, na kubadilishwa ili ukuwe muzuri. Kumbuka: uko huru kuamua kama moyo wako utafanana na udongo wa aina gani.

MUTU MWENYE TUNAPASWA KUPENDA ZAIDI

4. Ni sababu gani kubwa yenye itakuchochea ubatizwe?

4 Uko na mambo mingi ya muzuri yenye unapenda na kuona kuwa ya maana. Kwa mufano, pengine ulikuwa unaheshimia sana Biblia hata mbele uanze kujifunza na Mashahidi wa Yehova. Na pengine ulikuwa unamupenda Yesu kwa kadiri fulani. Sasa, kwa sababu umefikia kujua Mashahidi wa Yehova, pengine unapenda kujiunga nao. Lakini, haiko kupenda ile mambo ya muzuri tu njo kutakuchochea ujitoe kwa Yehova na kubatizwa. Sababu kubwa yenye itakuchochea ubatizwe ni kumupenda Yehova Mungu mwenyewe. Wakati unamupenda Yehova kupita mambo ingine yote, hautaruhusu kitu chochote ao mutu yeyote akuzuie kumutumikia. Kumupenda Yehova kutakuchochea ubatizwe na kutakusaidia pia uendelee kuwa muaminifu kwake kisha kubatizwa.

5. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

5 Yesu alisema kama tunapaswa kumupenda Yehova kwa moyo wetu wote, kwa nafsi yetu yote, kwa akili yetu yote, na kwa nguvu yetu yote. (Mk. 12:30) Unaweza kufanya nini ili umupende na kumuheshimia Yehova sana vile? Kufikiria namna Yehova anatupenda sana kunatuchochea tumupende pia. (1 Yo. 4:19) Katika habari hii tutazungumuzia mapendekezo fulani yenye itakusaidia kufanya vile. Pia, tutazungumuzia namna utajisikia na kutenda kisha kumupenda Yehova zaidi?b

6. Kulingana na Waroma 1:20, ni njia gani moja yenye inaweza kukusaidia ujifunze juu ya Yehova?

6 Ujifunze juu ya Yehova kwa kuchunguza vitu vyenye aliumba. (Soma Waroma 1:20; Ufu. 4:11) Fikiri sana juu ya mimea na wanyama wenye Yehova ameumba na namna vinaonyesha kama iko na hekima sana. Jifunze mambo fulani juu ya namna mwili wako umeumbwa kwa njia ya ajabu. (Zb. 139:14) Na ufikiri juu ya nguvu yenye Yehova alitia ndani ya jua letu, bila kusahau kama jua ni moja tu kati ya mamiliare ya nyota.c (Isa. 40:26) Wakati unafikiri juu ya vitu vyenye Yehova ameumba, utamuheshimia zaidi. Lakini, kujua kama Yehova iko na hekima na nguvu ni jambo moja tu kati ya mambo yenye inaweza kukusaidia ufanye urafiki pamoja naye. Kusudi umupende Yehova zaidi, unapaswa kujifunza mambo mingi juu yake.

7. Ili umupende Yehova zaidi, ni muzuri ukuwe hakika na jambo gani?

7 Ni muzuri ukuwe hakika kama Yehova anakuhangaikia kabisa. Ni nguvu kwako kuamini kama Muumbaji wa mbingu na dunia anajua kama uko na kama anakuhangaikia? Kama ni vile, kumbuka kama Yehova “haiko mbali sana na kila mumoja wetu.” (Mdo. 17:26-28) “Anachunguza mioyo yote,” na sawa vile Daudi alimuambia Sulemani, Yehova anakuahidi kwamba, “kama unamutafuta, atajiacha umupate.” (1 Ny. 28:9) Kwa kweli, kama uko unajifunza Biblia sasa, ni kwa sababu Yehova ‘amekuvuta kwake.’ (Yer. 31:3) Kadiri utaelewa zaidi mambo yote yenye Yehova amekufanyia, ni vile utamupenda zaidi.

8. Namna gani unaweza kumuonyesha Yehova kama unamupenda?

8 Njia moja ya kumuonyesha Yehova kama unamupenda ni kuzungumuza naye katika sala. Utamupenda Mungu zaidi wakati unaendelea kumuambia mambo yenye inakuhangaisha na kumushukuru juu ya mambo yote yenye anakufanyia. Na urafiki wako na Yehova utakuwa nguvu wakati utaendelea kuona namna anajibu sala zako. (Zb. 116:1) Utakuwa hakika kama anakuelewa. Lakini, kusudi umukaribie Yehova, unapaswa kuelewa namna anaona mambo. Na unapaswa kujua mambo yenye anataka ufanye. Njia moja tu ya kukusaidia ujue ile mambo yote ni kujifunza Biblia, Neno lake.

Wakati dada anauza vitu ku soko, anapatia trakte mwanamuke kijana mwenye kuuzisha mboga.

Njia ya muzuri zaidi ya kutusaidia tumukaribie Mungu na kujua mambo yenye anapenda tufanye ni kujifunza Biblia (Ona fungu la 9)d

9. Namna gani unaweza kuonyesha kama unaona Biblia kuwa ya maana?

9 Ujifunze kuona Biblia, Neno la Mungu, kuwa la maana. Ni Biblia tu njo iko na mafundisho ya kweli juu ya Yehova na mambo yenye amekusudia kufanya kwa ajili yako. Unaonyesha kama unaona Biblia kuwa ya maana kwa kuisoma kila siku, kwa kutayarisha funzo lako la Biblia, na kwa kutumikisha mambo yenye unajifunza. (Zb. 119:97, 99; Yoh. 17:17) Uko na programu ya kusoma Biblia kipekee? Unafuata ile programu, kwa kusoma Biblia kila siku?

10. Ni jambo gani moja lenye linafanya Biblia kuwa ya pekee?

10 Jambo moja kati ya mambo yenye kufanya Biblia ikuwe ya pekee ni hili: iko na habari zenye ziliandikwa na watu wenye walimuonaka Yesu. Biblia tu njo kitabu cha kweli chenye kinaonyesha mambo yenye Yesu amekufanyia. Wakati unaendelea kujifunza mambo yenye Yesu alisema na kufanya, utachochewa kuwa rafiki yake.

11. Ni nini inaweza kukusaidia umupende Yehova?

11 Ujifunze kumupenda Yesu, na utamupenda Yehova zaidi. Juu ya nini? Juu Yesu alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Njo maana, kadiri unajifunza zaidi juu ya Yesu, ni vile utafikia kujua muzuri zaidi mawazo ya Yehova na namna anatenda na utamukaribia zaidi. Fikiria namna Yesu alisikilia huruma watu wenye walikuwa wanazarauliwa, ni kusema, maskini, wagonjwa, ao wazaifu. Fikiria pia mashauri yenye kufaa yenye anakupatia na namna maisha yako inakuwa ya muzuri wakati unaifuata.​—Mt. 5:1-11; 7:24-27.

12. Wakati unajifunza juu ya Yesu, hilo linaweza kukuchochea ufanye nini?

12 Utamupenda Yesu zaidi wakati unaendelea kufikiri sana juu ya zabihu yenye alitoa ili Mungu asamehe zambi zetu. (Mt. 20:28) Wakati unaelewa kama Yesu alikuwa tayari kufa kwa ajili yako, jambo hilo linaweza kukuchochea utubu na kutafuta musamaha wa Yehova. (Mdo. 3:19, 20; 1 Yo. 1:9) Na wakati utafikia kumupenda zaidi Yesu na Yehova, utapenda zaidi kuwa pamoja na watu wenye wanawapenda pia.

13. Yehova amekupatia nini?

13 Ujifunze kupenda familia ya Yehova. Pengine watu wa familia yako wenye hawako Mashahidi na marafiki wako wa zamani hawataelewa juu ya nini unapenda kujitoa kwa Yehova. Wanaweza hata kukupinga. Yehova atakusaidia kwa kukupatia familia ya kiroho. Kama unaendelea kufanya urafiki na watu wa familia hiyo ya kiroho, watakuonyesha upendo na watakutolea musaada wenye uko nao lazima. (Mk. 10:29, 30; Ebr. 10:24, 25) Kisha wakati fulani, watu wa familia yako wanaweza kujiunga na wewe ili kumutumikia Yehova na kufuata kanuni zake.​—1 Pe. 2:12.

14. Kulingana na 1 Yohana 5:3, umetambua nini juu ya kanuni za Yehova?

14 Ujifunze kuheshimia kanuni za Yehova na kuzitumia mu maisha yako. Mbele ufikie kumujua Yehova, pengine ulijiwekea kanuni zako mwenyewe juu ya mambo ya muzuri na mambo ya mubaya, lakini sasa unaona kama kanuni za Yehova njo za muzuri. (Zb. 1:1-3; soma 1 Yohana 5:3.) Fikiria mashauri yenye Biblia inapatia bwana, bibi, wazazi, na watoto. (Efe. 5:22–6:4) Wakati unaendelea kutumia ile mashauri, umeona kama maisha ya familia yako imekuwa muzuri? Wakati unaendelea kutii maagizo ya Yehova juu ya namna ya kuchagua marafiki wako kwa hekima, tabia zako zimekuwa za muzuri? Uko mutu mwenye furaha zaidi? (Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33) Pengine unajibu ndiyo kwa ile maulizo.

15. Ni nini inaweza kukusaidia kujua namna ya kutumia kanuni za Biblia mu maisha yako?

15 Wakati fulani, unaweza kuona kama ni nguvu kujua namna ya kutumia kanuni za Biblia zenye uko unajifunza. Njo maana, kupitia tengenezo lake, Yehova anakupatia vichapo vyenye kutegemea Biblia vyenye vinaweza kukusaidia ujue mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. (Ebr. 5:13, 14) Wakati unasoma na kujifunza habari zenye kuwa katika vichapo hivyo, utaona kama kanuni za Biblia ni zenye kufaa kabisa na utajua namna ya kuzitumia mu maisha yako, na kwa hiyo, utapenda kuwa katika tengenezo la Yehova.

16. Namna gani Yehova amepanga watu wake?

16 Ujifunze kupenda na kutegemeza tengenezo la Yehova. Yehova amepanga watu wake katika makutaniko, na Yesu, Mwana wake, njo kichwa cha ile makutaniko yote. (Efe. 1:22; 5:23) Yesu ameweka kikundi kidogo cha wanaume watiwa-mafuta ili wasimamie mipango ya kazi yenye anapenda tufanye leo. Yesu aliita kikundi hicho cha wanaume “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” na wanakamata kwa uzito daraka lao la kutukulisha na kutulinda katika njia ya kiroho. (Mt. 24:45-47) Moja kati ya njia zenye mutumwa muaminifu anatumia ili kukuhangaikia ni kuweka katika kutaniko wazee wenye kustahili. Wanaweza kukuongoza na kukulinda. (Isa. 32:1, 2; Ebr. 13:17; 1 Pe. 5:2, 3) Wazee wako tayari kujitoa sana ili kukufariji, na kukusaidia uendelee kumukaribia Yehova zaidi. Lakini, jambo moja kati ya mambo ya maana zaidi yenye wanakufanyia, ni kukusaidia ili ujue kufundisha wengine juu ya Yehova.​—Efe. 4:11-13.

17. Kulingana na Waroma 10:10, 13, 14, juu ya nini tunazungumuza na wengine juu ya Yehova?

17 Usaidie wengine wamupende Yehova. Yesu aliambia wanafunzi wake wafundishe wengine juu ya Yehova. (Mt. 28:19, 20) Tunaweza kutii amri hiyo juu tu tunajua kama tunalazimika kufanya vile. Lakini, wakati unaendelea kumupenda Yehova zaidi, utajisikia kama vile mutume Petro na Yohana. Walisema hivi: “Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.” (Mdo. 4:20) Kusaidia mutu fulani afikie kumupenda Yehova njo jambo lenye kutuletea furaha zaidi. Wazia namna Filipo, mueneza-injili, alijisikia wakati alisaidia ule Muetiopia ajue kweli ya Maandiko na afikie kubatizwa! Wakati unamuiga Filipo na kutii amri ya Yesu ya kuhubiri, unaonyesha kama unapenda kuwa Shahidi wa Yehova. (Soma Waroma 10:10, 13, 14.) Kwa hiyo, pengine utajiuliza kama vile ule Muetiopia alijiuliza: “Ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?”​—Mdo. 8:36.

18. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

18 Utakamata uamuzi wa maana zaidi mu maisha yako wakati utaamua kubatizwa. Kwa sababu huo ni uamuzi muzito, unapaswa kufikiria kwa uangalifu maana ya uamuzi huo. Unapaswa kujua nini juu ya ubatizo? Unapaswa kufanya nini mbele na kisha kubatizwa? Tutajibu ile maulizo katika habari yenye kufuata.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni sababu gani kubwa yenye inapaswa kutuchochea tumutumikie Yehova, na juu ya nini unajibu vile?

  • Ni nini inaweza kukusaidia umupende Yehova?

  • Kufikiri sana juu ya mufano wenye kuwa katika Luka 8:11-15, kunaweza kutuletea faida gani?

WIMBO 2 Jina Lako Ni Yehova

a Watu fulani wanamupenda Yehova, lakini hawako hakika kama wako tayari kubatizwa ili kuwa Mashahidi wake. Kama unajisikia vile, habari hii itakusaidia uchunguze mambo fulani yenye unaweza kufanya ili ufikie kubatizwa.

b Kila mutu iko tofauti, kwa hiyo, watu fulani wanaweza kutumia mapendekezo ya habari hii kwa kufuata mupangilio tofauti na ule wenye kuonyeshwa katika habari hii.

c Ili kupata mifano zaidi, ona broshua Uhai​—Ulitokana na Muumba? na Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai.

d MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja anapatia trakte mwanamuke kijana mwenye anakutana naye mu duka.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine