Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/09/07
“Ningependa kujua wazo lako kuhusu jambo hili. [Soma Kumbukumbu la Torati 32:4.] Je, umekwisha kujiuliza kwa nini hapa duniani kuna mateso mengi na uovu mwingi hivi ikiwa Mungu ni mwenye uwezo wote na mwenye haki? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kwa nini Mungu anaruhusu uovu uendelee mpaka siku zetu.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Sisi wote tunapenda kuwa na afya njema na maisha marefu. Je, unafikiri kwamba kuwa na mawazo yenye kufaa kunaweza kufanya afya yetu iwe nzuri? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 17:22.] Habari hii inazungumzia kwa nini ni jambo linalofaa kutazamia mema.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 26.
Mnara wa Mlinzi 01/10/07
“Je, umekwisha kujiambia hivi, ‘Ninaona kwamba singepaswa kufanya hivyo!’? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo andiko hili linasema kuhusu sababu inayotufanya sisi wote, nyakati nyingine, tuchukue maamuzi yanayotusikitisha baadaye. [Soma Yeremia 10:23.] Gazeti hili linaeleza jinsi mashauri yanayofaa yanayopatikana katika Biblia yanatusaidia kufanya maamuzi mazuri.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Je, unafikiri kwamba leo kuna hatari zaidi kwa watoto kuliko wakati uliopita? [Acha mtu ajibu.] Wengi wanaona kwamba tunaishi katika siku zinazoelezwa hapa. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linatoa mapendekezo fulani yenye kufaa kuhusu jinsi wazazi wanavyoweza kulinda watoto wao na watu wanaovizia watoto ili kufanya nao ngono.”