Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Sept. 15
“Mamilioni ya watu wanaamini kwamba ‘watakatifu’ wana uwezo wa pekee na kwamba ni vizuri kusali kupitia wao. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo Yesu Kristo alisema. [Soma Yohana 14:6.] Jambo hilo linafanya watu fulani wajiulize ikiwa ni vizuri kusali kupitia ‘watakatifu.’ Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia habari hiyo ya maana.”
Amkeni! Sept. 22
“Wengi leo wana wasiwasi kuhusu ugaidi, kutia ndani matumizi ya silaha za kibiolojia. Je, unafikiri kwamba serikali za kibinadamu zinaweza kuondoa ugaidi ulimwenguni? [Acha mtu ajibu.] Biblia inaonyesha yale ambayo Mungu anakusudia kufanya. [Soma Ezekieli 34:28.] Amkeni! hii inazungumzia maswala fulani kati ya yale yanayohusika.”
MNARA WA MLINZI Okt. 1
“Wengi wanajiuliza ikiwa magumu yanayotuzunguka—vita, uhalifu, na matendo ya ugaidi—yatakuwa na mwisho. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Biblia inatoa uhakikisho huu wenye kufariji. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili linaeleza kwa nini Mungu hajamaliza uovu na kuteseka kunakotokana nao.”
Amkeni! Okt. 8
“Leo inaonekana kwamba kuna ongezeko kubwa katika hesabu ya familia zenye mzazi mmoja. Biblia inaonyesha kwamba Muumba wetu ni mwenye huruma kwa ajili ya familia hizo. [Soma Zaburi 146:9.] Toleo hili la Amkeni! linaonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kusaidia wazazi wasio na mwenzi wa ndoa walee watoto wao kwa mafanikio.”