Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Mamilioni ya watu wanatumia maneno haya yenye kujulikana sana katika sala zao. [Soma Mathayo 6:10.] Unafikiri maisha yangekuwaje ikiwa mapenzi ya Mungu yalitimizwa kikamili duniani? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia maana ya kila sehemu ya Sala ya Bwana, kutia ndani sehemu ambayo tumesoma sasa hivi.”
Amkeni! Sept. 22
“Watu wengi wana wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa tatizo moja kati ya vijana—ulevi. Je, umekwisha kusikia kuhusu hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 20:1.] Ulevi unatia vijana katika hatari nyingi. Makala hii ina habari inayoweza kuwasaidia washinde mkazo wa matumizi mabaya ya pombe.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Sisi sote tunatazamia sana kuona mwisho wa uhalifu, jeuri, na vita. Je, unafikiri kwamba tutapata kuona utimizo wa maneno haya? [Soma Zaburi 37:11. Kisha uache mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ahadi hii inavyohusiana na kusudi la Mungu la hapo mwanzoni kwa ajili ya wanadamu na jinsi tunavyoweza kushiriki katika kusudi hilo.”
Amkeni! Okt. 8
“Ni jambo lenye huzuni kuona kwamba kila mwaka mamilioni ya wasichana wasioolewa wanachukua mimba, sivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia hatua wanazoweza kuchukua ili kupambana na matatizo mengi ya umama wakiwa bado vijana. Inazungumzia pia jinsi wazazi wanavyoweza kusaidia watoto wao ili waepuke kwanza tatizo hilo.” Soma 2 Timotheo 3:15.