Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/08 uku. 1
  • “Chukueni Nira Yangu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Chukueni Nira Yangu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Alitolea Watu Kitulizo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • “Mukuje Kwangu, . . . na Mimi Nitawapumuzisha”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kazi Inayoburudisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 5/08 uku. 1

“Chukueni Nira Yangu”

1 Katika ulimwengu huu wenye kujaa mikazo na mahangaiko, tumetulizwa kwelikweli kwa kukubali mwaliko wa Yesu wenye shauku ili kupata burudisho tunapochukua nira yake. (Mt. 11:29, 30) Kukubali nira ya kuwa mwanafunzi wa Yesu kunatia ndani kufanya kazi ambayo si ngumu tu lakini pia yenye kuburudisha. Kazi hiyo inahusisha kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuwasaidia wengine kupata kiburudisho pamoja nasi tunapochukua nira ya Yesu.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Furaha Inayotokana na Mahubiri: Yesu hakuomba wafuasi wake waongeze mzigo wake kwenye mizigo wayolikuwa nayo. Aliwaomba wamutolee mizigo yao mizito na kuchukua mzigo wake mwepesi. Hatuna tena mizigo ya mahangaiko na ukosefu wa tumaini vinavyotokana na ulimwengu huu; pia hatutumiki kwa ajili ya utajiri usio hakika. (Luka 21:34; 1 Tim. 6:17) Ijapokuwa tuna kazi nyingi na tunapaswa kutumika ili kutosheleza mahitaji yetu ya kila siku, tunatia pa nafasi ya kwanza ibada ya Mungu katika maisha yetu. (Mt. 6:33) Wakati wote tutaona kazi ya kuhubiri kuwa yenye kuleta furaha, wala si mzigo mzito, ikiwa tunaendelea kuwa na maoni mazuri kuhusu mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.

3 Kwa kawaidia, tunafurahia kuzungumzia jambo lolote la maana sana lililo katika moyo wetu. (Luka 6:45) Mambo ambayo ni ya maana sana kwa Wakristo wote yanahusu Yehova na baraka za Ufalme ambazo ameahidi. Kwa hiyo, ni jambo lenye kufurahisha kabisa kuzungumzia “habari njema ya mambo mazuri” na kusahau mahangaiko yetu ya kila siku tunapohubiri. (Rom. 10:15) Kwa kweli, kadiri tunavyoendelea kufanya jambo fulani, ndivyo tunakuwa na uwezo wa kulifanya na tunapata furaha nyingi. Kwa hiyo, kupitisha wakati mwingi katika mahubiri, ikiwa tuna uwezo, kutatuletea furaha nyingi. Na inafurahisha kabisa kuona watu wakikubali mambo tunayowahubiria. (Mdo. 15:3) Hata tunapokutana na watu wasiopendezwa na mambo tunayowafundisha ao upinzani, kazi ya kuhubiri inaleta burudisho la kiroho ikiwa tunakumbuka kwamba bidii yetu inamfurahisha Yehova na kwamba matokeo mazuri yoyote tunayopata ni baraka kutoka kwake.—Mdo. 5:41; 1 Kor. 3:9.

4 Kwa kukubali mwaliko wa Yesu, tunapata pendeleo la kutumika pamoja naye kama Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10; Ufu. 1:5) Hakuna jambo linaloweza kufurahisha kabisa kama hilo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine