Wahubiri wa Ufalme Wapendwa:
Tunafurahi sana kuwatolea ripoti ya utumishi wa shambani ya mwezi wa 3, 2008. Katika Congo-Kinshasa tulifikia hesabu mpya ya wahubiri 150,309. Katika inchi hii, hiyo ni mara ya kwanza ambayo wahubiri zaidi ya 150,000 wanatoa ripoti zao katika mwezi mmoja. Kulikuwa pia hesabu mpya ya saa zilizopitishwa katika mahubiri, katika kuongoza mafunzo ya Biblia, na katika sehemu zingine za kazi ya kuhubiri. Zaidi ya hilo, tulifurahi kuona kwamba wahubiri wenye bidii 5,174 katika Congo-Brazzaville walifikia hesabu mpya ya saa 122,365 katika kazi ya kuhubiri. Tunataka kuwapongeza (féliciter) nyinyi wote kwa ajili ya bidii yenu katika kazi ya kuhubiri habari njema.—1 Kor. 15:58.
Kazi ya ujenzi inaendelea vizuri kwenye biro ya Tawi. Tarehe 28 mwezi wa 4, 2008, familia ya Betheli ilifurahi kuanza kutumia chumba kipya cha kulia chakula na chumba kipya cha kupikia chakula. Chumba kipya cha kulia chakula ni kikubwa mara mbili kupita kile cha kwanza, na kina nafasi kwa ajili ya watu 600.
Siku ya Posho tarehe 23 mwezi wa 2, 2008, Jumba la Mikusanyiko huko Limete, Kinshasa liliwekwa wakfu. Wahuzuriaji wote walikubali kwa furaha kutumia jumba hilo na kulitunza ili kumletea Yehova sifa. Katika mwezi wa 7, Jumba lingine la Mikusanyiko lilimalizwa huko Kisangani na kuna mipango ya kujenga majumba mengine huko Lubumbashi na Mbuji-Mayi wakati ujao ulio karibu. Kwa kuongezea, viwanja vya mikusanyiko viliwekwa wakfu huko Beni mwezi wa 2, 2008 na huko Butembo mwezi wa 4, 2007. Tunafurahi sana kwa kuwa majengo hayo yanatumiwa ili kumletea Yehova sifa.
Basi, na tuendelee kusimama imara tunapongojea wokovu ambao unakaribia sana kutoka kwa Yehova.
Ndugu zenu,
Biro ya Tawi la Congo-Kinshasa