Kisanduku Cha Maulizo
◼ Je, wazazi wote wawili wanaweza kuhesabu saa zinazotumiwa wakati wa funzo la familia la kawaida?
Ijapokuwa baba ndio walio na daraka kwanza la kulea watoto wao katika “nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova,” wazazi wote wawili wanashiriki katika kuzoeza watoto wao. (Efe. 6:4) Biblia inaonya watoto hivi: “Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako.” (Met. 1:8) Funzo la Biblia la familia ni njia moja ya maana ambayo wazazi wanatumia ili kuzoeza watoto wao.
Wakati uliopita, mzazi aliyeongoza funzo la familia na watoto wasiobatizwa ndiye alihesabu saa, hata ikiwa wazazi wote wawili walishiriki katika mazungumzo. Lakini, jambo hilo linarekebishwa. Ikiwa wakati wa funzo la familia wazazi wote wawili wanashiriki katika kufundisha watoto, hivyo, wote wawili wanaweza kuhesabu wakati usiozidi saa moja kila juma kwa ajili mahubiri. Ni wazi kwamba wazazi wanatumia mara nyingi zaidi ya saa moja kila juma kwa kufundisha watoto wao. Inaomba wazazi wote wawili waendelee kujikaza ili kuzoeza watoto. (Kum. 6:6-9) Hata hivyo, ripoti ya mahubiri ya kila mwezi inapaswa kuonyesha kwanza kazi inayofanywa katika shamba. Kwa hiyo, hawapaswi kuhesabu zaidi ya saa moja kila juma hata ikiwa funzo limeongozwa zaidi ya mara moja kwa juma ao hata ikiwa wanajifunza na mtoto mmoja-mmoja. Ni mzazi mmoja tu anayepaswa kuripoti funzo la Biblia la familia na kuhesabu ziara za kurudia kila juma wanapoongoza funzo.