Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 2 uku. 4-5
  • Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Ufalme wa Mungu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Ufalme wa Mungu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UTAWALA WA WANADAMU UNATOKEA
  • WAKATI WA KUTENDA!
  • Juu ya Nini Kuko Mateso na Mambo Mingi ya Mubaya?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Juu ya Nini Mungu Anaacha Mambo ya Mubaya na Mateso Iendelee?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Mungu Anapenda Wanadamu Wakuwe na Maisha ya Namna Gani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 2 uku. 4-5
Adamu na Eva wako wanaangalia namna maji iko inashuka kutoka juu katika bustani ya Edeni

Chini ya utawala wa Mungu, uumbaji wote ulikuwa katika umoja na amani

Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Ufalme wa Mungu?

Ku mwanzo wa historia ya wanadamu, Muumbaji wetu, mwenye jina lake ni Yehova, njo tu mwenye alikuwa Mutawala. Alitawala kwa upendo. Alifanya makao ya muzuri sana, ni kusema, bustani katika Edeni, ili watu waishi ndani. Aliwapatia pia chakula mingi. Tena, alipatia wanadamu kazi ya muzuri sana. (Mwanzo 1:28, 29; 2:8, 15) Wanadamu wangeendelea kuwa na amani kama wangemuacha Mungu mwenye upendo aendelee kuwatawala.

Adamu iko anakamata tunda lenye Eva anamuletea lenye waliwakataza

Wanadamu wa kwanza walimukataa Mungu kuwa Mutawala wao

Biblia inasema kama malaika mumoja muasi, mwenye alifikia kuitwa Shetani Ibilisi, alisema kama Mungu hana haki ya kutawala wanadamu. Kwa njia fulani, alisema kama wanadamu watakuwa na furaha zaidi bila kuongozwa na kutawaliwa na Mungu. Jambo la kuhuzunisha, wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, walimufuata Shetani na wakamuasi Mungu.​—Mwanzo 3:1-6; Ufunuo 12:9.

Kwa sababu Adamu na Eva walimukataa Mungu kuwa Mutawala wao, walipoteza makao yao ya Paradiso na tumaini la kuishi milele wakiwa na afya kamilifu. (Mwanzo 3:17-19) Uamuzi wao ulikuwa pia na matokeo kuhusu watoto wenye walifikia kuzaa. Biblia inasema kama kwa sababu Adamu alifanya zambi, “zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi.” (Waroma 5:12) Zambi ilileta matokeo ingine ya mubaya: “Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Ile inamaanisha kama, wakati wanadamu wanajiongoza wao wenyewe, lazima tu magumu ikuwe mingi.

UTAWALA WA WANADAMU UNATOKEA

Nimrodi anasimama akiwa na sura ya kujivuna. Nyuma yake, watu wako wanajenga nyumba.

Nimrodi alimuasi Yehova

Mutawala wa kwanza mwanadamu mwenye kutajwa katika Biblia ni Nimrodi. Alipinga utawala wa Yehova. Kuanzia siku za Nimrodi, wanadamu wenye nguvu wametumia mamlaka yao mubaya. Karibu miaka 3000 yenye imepita, Mufalme Sulemani aliandika hivi: “Nikaona machozi ya wenye kukandamizwa, na hapakukuwa mutu wa kuwafariji. Na wakandamizaji wao walikuwa na nguvu.”​—Muhubiri 4:1.

Ni vile pia leo. Katika mwaka wa 2009, kichapo kimoja cha Umoja wa Mataifa kilisema kama utawala mubaya unaendelea kuonekana kuwa “sababu moja kati ya sababu mingi zenye kufanya mambo ya mubaya ifanyike katika ulimwengu leo.”

WAKATI WA KUTENDA!

Ulimwengu uko na lazima ya watawala wazuri na serikali ya muzuri. Na hilo njo jambo lenye Muumbaji wetu ameahidi!

Picha: Matokeo ya utawala wa wanadamu. 1. Mwanamuke mumoja wa Asia iko anakaa kwenye barabara yenye kuchafuka na iko na mutoto wake mwenye iko analia. 2. Muzee mumoja mwenye kuwa mugonjwa iko ku kitanda katika hopitali. 3. Waaskari wako wanapiga bunduki zao katika eneo la vita. 4. Watu wenye kasirani wenye kufanya maandamano, wako wanalalamika na wako na bendera. 5. Mwanamuke mumoja pamoja na mutoto wake mwanamuke wako wanasimama inje ya nyumba yao, na wanaona kuwa kioo ya mulango wao ilisha kuvunjika. 6. Muji mumoja wenye kujaa kunguku na tuyaux za kupitishia moshi na kamba za umeme.

Hata serikali za muzuri zaidi za wanadamu zimeshindwa kumaliza matatizo makubwa ya wanadamu

Mungu amesimamisha Ufalme ao serikali, yenye itakamata nafasi ya serikali zote za wanadamu, na “ufalme huo peke yake utasimama milele.” (Danieli 2:44) Njo Ufalme wenye mamilioni ya watu wamekuwa wakiomba. (Matayo 6:9, 10) Lakini Mungu hatatawala yeye mwenyewe. Ameweka mutu fulani mwenye aliishi kama mwanadamu ili akuwe Mutawala. Ni nani mwenye Mungu amechagua?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine