Kisanduku Cha Maulizo
◼ Mashirika ya kisheria yanayotumiwa na Mashahidi wa Yehova yana alama zinazoyatambulisha. Je, makutaniko ao watu wanaweza pia kutumia alama hizo?
Kitambulisho kinaweza kuwa jina, alama ao cachet inayotumiwa na shirika fulani ili kujitambulisha kwa urahisi, kitambulisho hicho hakiwezi kutumiwa na shirika lingine. Alama ya mnara inayopatikana kwenye gazeti Mnara wa Mlinzi ndiyo alama ya kitambulisho ya shirika Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania na mashirika mengine yanayotumiwa na tengenezo. Kwenye sehemu ya juu ya barua zake, shirika Christian Congregation of Jehovah’s Witnesses linatumia Biblia yenye kufunguliwa kama alama ya kitambulisho. Mashirika mengine yanayotumiwa na Mashahidi wa Yehova yana alama tofauti tofauti.
Makutaniko ao watu hawapaswi kutumia alama za vitambulisho ao majina ya mashirika ya kisheria ya tengenezo ao majina na vitambulisho vingine vyenye kufanana na hivyo ili kutambulisha Majumba yao ya Ufalme, kwenye barua zao, kwenye vitu vya pekee vya mutu, na kazalika. Kutumia alama inayotambulisha tengenezo kwa njia hiyo kunaweza kuvuruga maofisa wa serikali, wahubiri, na watu wengine kuhusu uhusiano ulio kati ya kutaniko na mashirika ya kisheria yanayotumiwa na tengenezo. Vivyo hivyo, wengine wanaweza kufikiri kimakosa kwamba barua zilizo na alama hizo za kutambulisha tengenezo zimekubaliwa ao kutumwa na makao makuu ya Mashahidi wa Yehova ao na biro ya tawi.
Alama hiyo ya mnara, ao alama nyingine yenye kufanana na kitambulisho hicho, havipaswi kutumiwa kwenye Majumba ya Ufalme yatakayojengwa wakati ujao hata ikiwa Jumba la Ufalme limeandikishwa kwa jina la shirika fulani la Watch Tower. Makutaniko yaliyo na Majumba ya Ufalme yenye kuwa na alama inayotambulisha tengenezo hayaombwi kuibadili mara moja, kwa kuwa kufanya hivyo kunaweza kuhusisha kazi nyingi na wakati mwingi, nguvu nyingi na feza nyingi. Hata hivyo, makutaniko yatafikiria kubadili alama hiyo ikiwa ni badiliko ndogo tu ambalo halitaomba kazi nyingi. Kama sivyo, badiliko linaweza kufanywa wakati ambapo kutakuwa mpango wa kutengeneza upya Jumba la Ufalme.