Je, Unaweza Kufanya Mengi Zaidi Katika Kazi ya Kuhubiri?
1. Kuna uhitaji gani wa kutenda kwa haraka katika kazi ya kuhubiri, na kwa nini?
1 Yesu alipoona kwamba watu wengi sana walipendezwa na habari njema ya Ufalme, aliwaagiza wanafunzi wake ‘wamwombe Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.’ (Mt. 9:37, 38) Kwa kuwa tunakaribia sana mwisho wa kipindi cha mavuno, kazi yetu inahitaji kufanywa kwa haraka kuliko wakati mwingine wowote. Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kufikiria katika sala jinsi tunavyoweza kufanya mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri.—Yoh. 14:13, 14.
2. Namna gani wahubiri fulani wamekubali mwaliko wa kutafuta wafanyakazi wengi zaidi katika shamba?
2 Njia Mbalimbali za Kufanya Mengi Zaidi Katika Kazi ya Kuhubiri: Kwa mwongozo na msaada wa Yehova, wengi wameona kwamba wanaweza kufanya kazi ya upainia. (Zab. 26:2, 3; Flp. 4:6) Wengine walijikaza kwa njia ya pekee ili kuwa mapainia wasaidizi mwezi mmoja ao zaidi katika mwaka. Hiyo ilionekana kuwa njia nzuri zaidi ya kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri. Furaha inayotokana na kazi ya upainia msaidizi imechochea wengi kati yao wafikirie kuwa mapainia wa kawaida.—Mdo. 20:35.
3. Ikiwa ulifanya kazi ya upainia wakati uliopita, ni jambo gani unaloweza kufikiria sasa?
3 Je, Unaweza Kurudilia Kazi ya Upainia?: Ikiwa ulifanya kazi ya upainia wakati uliopita, bila shaka unaendelea kukumbuka mambo yenye kufurahisha ya wakati huo. Je, umefikiria katika sala ikiwa unaweza kurudilia tena kazi ya upainia? Labda hali zilizokufanya uache upainia hazitakuzuia tena. Inaweza kuwezekana sasa urudilie tena pendeleo hilo la pekee.—1 Yoh. 5:14, 15.
4. Ni nafasi gani ya pekee tulio nayo sisi wote?
4 Kazi ya mavuno inaendelea na karibuni itafikia mwisho. (Yoh. 4:35, 36) Sisi wote na tuchunguze hali yetu ya sasa ili kuona ikiwa tunaweza kupanga programu yetu vizuri kusudi tufanye mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri. Ao ikiwa kwa kweli haiwezekane kwetu kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri, je, tunaweza kutafuta njia mbalimbali zinazoweza kutusaidia ili tupate matokeo mazuri zaidi? (Marko 12:41-44) Ni pendeleo nzuri zaidi linalotiwa sasa mbele ya wale wote ambao hali zao zinawaruhusu watumiwe na Yehova katika utumishi huo wa pekee!—Zab. 110:3.