Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/09 uku. 3
  • Tumsifu Yehova Kila Siku

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumsifu Yehova Kila Siku
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumusifu Yehova Mungu Wetu!
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
  • Tubariki Yehova “Mchana Kutwa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Yehova Anastahili Kusifiwa Sana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • “Musifu Jina la Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 7/09 uku. 3

Tumsifu Yehova Kila Siku

1. Watumishi wa Mungu wanachochewa kufanya nini, na kwa nini?

1 Mfalme Daudi alionyesha kusudi lake la kumsifu Yehova “mchana kutwa,” hata milele. (Zab. 145:2, 7, 21) Sisi pia tuna sababu nzuri ya kumsifu Yehova kila siku.—Zab. 37:10; 145:14, 18; 2 Pet. 3:13.

2. Namna gani watu wa familia wanaweza kumsifu Yehova kila siku?

2 Tumsifu Yehova Nyumbani Mwetu: Tuna vitabu vilivyo na habari zenye kujenga tunazotumia katika mazungumzo ya kiroho ya maana tunapochunguza andiko la siku, tunapofanya Ibada ya Familia na tunapotayarisha mikutano ya kutaniko. Watu wa familia nyingi wanazoea kula chakula pamoja hata mara moja kwa siku. Wanapokula pamoja wanapata nafasi ya kuzungumza vizuri wakiwa wenye kutulia, na wanapata nafasi za kumsifu Yehova. Mazungumzo ya kirafiki kama hayo yanayoanzishwa na wazazi yanaweza kusaidia kabisa wazazi ili kulea watoto katika “nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.”—Efe. 6:4; Kum. 6:5-7.

3. Tunapokuwa na ndugu zetu, tuna nafasi gani za kumsifu Yehova?

3 Tumsifu Yehova Pamoja na Ndugu Zetu: Tunapokuwa katika mahubiri ao kwenye mikutano ya kutaniko, tuna nafasi nzuri zaidi za kumsifu Yehova pamoja na ndugu zetu. (Met. 15:30; Flp. 4:8; Ebr. 13:15) Kwa kuwa sisi wote tunampenda Yehova, haitakuwa vigumu kwetu tunapozungumza na wengine, kutia katika mazungumzo yetu maneno ya shukrani yanayotoka moyoni kuhusu wema wa Yehova.—Zab. 106:1.

4. Hata ikiwa hatukuenda katika mahubiri, ni katika hali gani zingine tunaweza kumsifu Yehova?

4 Tumsifu Yehova Tunapozungumza na Watu Wasio Mashahidi: Hata ikiwa hali mbalimbali zinaweza kutuzuia kwenda katika mahubiri kila siku, kuzungumza kumhusu Yehova na makusudi yake hata kwa dakika chache pamoja na wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu na watu wengine walio karibu nasi kunaweza kuwafanya watu wenye mioyo ya haki wawe na tumaini. (Zab. 27:14; 1 Pet. 3:15) Dada mmoja aliyekuwa akisafiri kwa ndege alimhubiria msafiri mwenzake ambaye alifarijiwa sana na kutiwa moyo na mambo aliyosikia hivi kwamba alimpatia dada adresi yake na namba ya telefone ili waendelee kupashana habari. Wakati ambapo watu wa ulimwengu wanasumbuliwa kwa sababu ya kuongezeka kwa taabu na hali mbaya, watu wa Yehova wanaendelea kutolea wale walio tayari kusikiliza “habari njema za jambo bora”. Hilo linawapa wengine tumaini na nafasi ya kumsifu Yehova.—Isa. 52:7; Rom. 15:11.

5. Kwa nini tuna nia ya kumsifu Yehova, na hilo linaweza kuwa na matokeo gani?

5 Bila shaka, Yehova anapendezwa sana anaposikia watumishi wake wanamsifu kila siku! Kama vile vitu vinavyoonekana vyenye kutuzunguka ambavyo ni uumbaji wa Yehova, sisi pia tunaweza kumsifu kila siku nyumbani mwetu, katika kutaniko, na tunapozungumza na wengine ambao hawajaanza kumsifu Yehova.—Zab. 19:1-4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine