Tujikaze Kuhubiria Wanaume
1. Kuna uhitaji gani mkubwa ili kuendeleza faida za Ufalme?
1 Kwa kuwa kazi ya Ufalme inaendelea kuongezeka katika siku hizi za mwisho, kuna uhitaji mkubwa wa wanaume wenye kukomaa kiroho ili kuongoza. (Marko 4:30-32; Mdo. 20:28; 1 Tim. 3:1-13) Hata hivyo, katika sehemu fulani wanaume wanaokubali ujumbe wa Ufalme ni wachache kuliko wanawake. Kulingana na desturi fulani, wanaume wanafikiri kwamba ni daraka la wanawake kufundisha watoto Neno la Mungu. Namna gani tunaweza kuwasaidia wanaume wengi watambue mahitaji yao ya kiroho na kujiunga nasi katika ibada ya kweli?
2. Namna gani Paulo na Petro walipata matokeo mazuri walipojikaza kuwatolea wanaume ushahidi?
2 Tutafute Nafasi ya Kuhubiri Wanaume: Mara nyingi, baba wa familia anapokubali kweli, anachochea familia yote ijiunge naye katika ibada safi. Kwa mfano, walipokuwa katika kifungo kwa sababu ya kuhubiri, Paulo na Sila walimtolea mlinzi wa gereza ushahidi. Mlinzi huyo pamoja na familia yake yote walibatizwa. (Mdo. 16:25-34) Huko Korintho, Paulo alihubiria “Krispo ofisa-msimamizi wa sinagogi akawa mwamini katika Bwana, na ndivyo na watu wote wa nyumba yake.” (Mdo. 18:8) Yehova alimtuma Petro ili kumtolea ushahidi Kornelio ofisa wa jeshi, aliyeelezwa kuwa “mtu mwenye kuheshimu na kumwogopa Mungu.” Kornelio pamoja na familia yake na marafiki zake wa karibu walibatizwa.—Mdo. 10:1-48.
3. Kwa kufuata mfano wa Filipo, ni watu gani walio katika “cheo cha juu” ambao unaweza kutolea ushahidi?
3 Kutolea ushahidi wanaume “wenye cheo cha juu” kunaweza kuwa na matokeo mazuri sana. (1 Tim. 2:1, 2) Kwa mfano, malaika wa Yehova alimshauria Filipo azungumze na “mwanaume aliye na mamlaka” ambaye alilinda hazina zote za malkia wa Etiopia. Filipo alimsikiliza mwanaume huyo “akimsoma kwa sauti kubwa Isaya” na akamtolea habari njema kuhusu Yesu. Mwetiopia huyo akawa mwanafunzi, na labda aliporudi nyumbani alitangazia watu habari njema. Pia, labda alimtolea malkia ushahidi na wote waliokuwa katika makao yake, watu ambao ilikuwa vigumu kukutana nao ili kuwatolea habari njema.—Mdo. 8:26-39.
4. Namna gani tunaweza kuwasaidia wanaume wapate nafasi za kusikiliza habari njema?
4 Jinsi ya Kuwapata Wanaume Wengi: Kwa kuwa mara nyingi wanaume wanapatikana kwenye nafasi za kazi mchana, je unaweza kupanga programu yako ili upitishe wakati mwingi katika mahubiri magaribi, Siku ya Posho na Siku ya Yenga, ao wakati wa mapumziko? Kuhubiri kwa ukawaida mahali pa biashara, kutakutolea nafasi nyingi ya kutolea ushahidi wanaume ambao hawapatikani nyumbani mara nyingi. Pia, ndugu wanaweza kujikaza ili kuhubiria wafanyakazi wenzao wanaume wakati hawakupanga kufanya hivyo. Katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, zaidi sana katika eneo ambalo linahubiriwa mara nyingi, ndugu wanaweza kuomba kuzungumza na bwana wa nyumba.
5. Dada atafanya nini ikiwa anahubiri mwanaume anayependezwa na ujumbe wa Ufalme?
5 Ikiwa dada anahubiria mwanaume fulani, naye anapendezwa na ukweli, hapaswi kumrudilia akiwa pekee yake. Anaweza kumrudilia akiwa na mume wake ao mhubiri mwingine. Mwanaume huyo anapofanya maendeleo, kwa kawaida ni vizuri zaidi kumwachia ndugu mwenye kukomaa kiroho aendelee kumsaidia.
6. Namna gani tunaweza kumwiga mtume Paulo ili ‘tupate watu wengi’?
6 Tafuta Habari Zinazopendeza Wanaume: Mtume Paulo alifikiria wasikilizaji wake na kuambatanisha mafundisho yake na hali zao ili ‘kuwapata watu wengi.’ (1 Kor. 9:19-23) Sisi pia, tunapaswa kufikiria habari zinazoweza kuchochea wanaume ambao tunaweza kukutana nao, na kujitayarisha vizuri. Kwa mfano, mara nyingi wanaume wanapendezwa na habari zinazohusu matatizo ya kupata feza, serikali nzuri, na usalama wa familia zao. Wanaweza kupendezwa pia na habari zinazohusu kusudi la maisha, wakati ujao wa dunia, na kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka. Ikiwa tunafikiria mambo hayo tunapowatolea wanaume ujumbe wa Ufalme, tutapata matokeo mazuri.—Met. 16:23.
7. Namna gani washiriki wote wa kutaniko wanaweza kuwasaidia waume wasioamini wanaohuzuria mikutano?
7 Chukua Hatua ya Kuhubiri Waume Wasioamini: Ijapokuwa mwenendo safi wa wake Wakristo mara nyingi unavutia sana waume wao wasioamini, washiriki wa kutaniko wanaweza pia kusaidia. (1 Pet. 3:1-4) Wakati mume asiyeamini anapomsindikiza muke wake kwenye mkutano, akikaribishwa vizuri na kutaniko, hilo litamtolea ushahidi wenye nguvu. Kuwapo kwake kwenye mkutano kunaweza kuonyesha kwamba anapendezwa na kweli kwa kiasi fulani, na kwamba anaweza kukubali funzo la Biblia.
8. Ndugu wanaweza kufanya nini ili kuwasaidia waume wasioamini ambao wameonyesha kupendezwa na kweli kwa kiasi kidogo?
8 Kwa upande mwingine, waume fulani, mwanzoni wanaweza kupendezwa kwa kiasi kidogo na mambo ya Biblia, lakini mwishowe wanaweza kukubali mazungumzo kuhusu Biblia pamoja na ndugu ambaye wanapendezwa naye. Katika kutaniko moja, ndugu walijikaza kutembelea familia iliyogawanyika kidini na kuzungumza na mume asiyeamini kuhusu mambo ambayo walijua anapendezwa nayo. Hilo lilifanya kuwe na mazungumzo ya Biblia kati yao, na sasa mume huyo ni mwenye kubatizwa. Mfano mwingine, ndugu mmoja alimsaidia mume asiyeamini aliye na hali ya urafiki, kujenga pango ya nyumba yake. Kwa kuwa ndugu alionyesha kupendezwa naye, mume huyo alikubali waanze kujifunza Biblia. (Gal. 6:10; Flp. 2:4) Ikiwa wewe ni ndugu, kwa nini usichukue hatua ya kumhubiri mume mmoja asiyeamini ao wengi?
9. Kuzoeza wanaume Wakristo kunaweza kuwa na matokeo gani?
9 Kuwazoeza Wanaume Wakristo: Wanaume wanaokubali ujumbe wa Ufalme na kujikaza kufikia mapendeleo ya kitheokrasi katika utumishi wa Mungu, wanaweza kufikia kuwa “zawadi katika wanadamu;” yaani wazee Wakristo ambao wanatumia uwezo na nguvu zao kwa ajili ya kutaniko la watu wa Yehova. (Efe. 4:8; Zab. 68:18) Wanaume hao wanachunga kutaniko kwa kujipendea. (1 Pet. 5:2, 3) Wanakuwa baraka kabisa kwa ushirika mzima wa ndugu!
10. Namna gani bidii ya Anania ya kumsaidia Paulo iliwafaidi watu wengi?
10 Kwa mfano, Paulo alikuwa “mtume kwa mataifa,” ijapokuwa hapo mbele alikuwa akiwatesa Wakristo. (Rom. 11:13) Mwanzoni, mwanafunzi Anania alisita kumhubiria Paulo kwa sababu alijua kwamba aliwatesa Wakristo. Hata hivyo, Anania alifuata mwongozo wa Bwana na akazungumza na mwanaume huyo ambaye mwishowe akawa mtume Paulo. Baada ya miaka, watu wengi walifaidika na mahubiri ya Paulo. Pia, watu wengi wanaendelea kufaidika na barua zilizoongozwa na roho ambazo Paulo aliandika zinazopatikana katika Biblia.—Mdo. 9:3-19; 2 Tim. 3:16, 17.
11. Kwa nini tufanye mabadiliko yanayohitajiwa ili kuwahubiria wanaume?
11 Basi, na tufanye mabadiliko yanayohitajiwa ili kujikaza kuhubiria wanaume. Ikiwa tunafuatia kusudi hilo, tuko hakika kwamba Yehova atatubariki tunapojikaza kufanya mapenzi yake na kushugulikia vizuri faida za Ufalme.