Tuwarudilie Wale Wenye Kupendezwa—Wakati Gani?
1. Kazi ya kufanya wanafunzi inahusisha nini?
1 Kazi ya kufanya wanafunzi inahusisha kumrudilia mutu yeyote anayeonyesha nia ya kujifunza kuhusu Ufalme wa Yehova. (Mt. 28:19, 20) Mara nyingi, wakati unaofaa zaidi ili kumrudilia mutu unategemea programu yetu na ile ya mutu mwenye kupendezwa. Kwa nini tumrudilie mutu bila kukawia kisha kumhubiria kwa mara ya kwanza?
2, 3. Kwa nini tujikaze kumrudilia mutu bila kukawia?
2 Kwa Nini Turudi Bila Kukawia? Kazi ya kuhubiri “hii habari njema ya Ufalme” inakaribia kumalizika na ulimwengu huu unakaribia kufikia mwisho wake. (Mt. 24:14; 1 Pet. 4:7) Kwa hiyo, kwa kuwa wale wenye kupendezwa wangali na nafasi ya kufaidika na “siku ya wokovu,” tunapaswa kutii shauri la ‘kuhubiri neno kwa bidii,’ hilo linamaanisha pia kuwarudilia watu haraka iwezekanavyo ili kuwasaidia waendelee kupendezwa zaidi.—2 Kor. 6:1, 2; 2 Tim. 4:2.
3 Shetani iko tayari kuondoa mbegu yoyote ya Ufalme ambayo tunaweza kupanda ndani ya moyo wa mutu mwenye kupendezwa. (Marko 4:14, 15) Mara nyingi, watu wanaoonyesha kupendezwa wanazihakiwa na watu wa familia zao, wafanyakazi wenzao na watu wengine. Kuwarudilia bila kukawia kunatuwezesha tuendeleshe mazungumzo mbele watu wengine wawavunje moyo.
4. Tunapomhubiria mutu kwa mara ya kwanza, tunaweza kufanya nini ili kumtayarisha kwa ajili ya mazungumzo ya wakati ujao?
4 Tupange Wakati wa Kurudi: Ni vizuri zaidi kupanga wakati wa kurudilia mutu mbele ya kuachana naye tunapomhubiria kwa mara ya kwanza. Tutokeze ulizo ambalo tutajibu tunaporudia. Ni jambo la maana kuandika mambo fulani tunapoonana na mutu kwa mara ya kwanza na kuhusu wakati tunaopanga kukutana tena. Ikiwa programu yetu inaturuhusu, tunaweza kumwuliza ikiwa inawezekana kumrudilia siku inayofuata ao muda mfupi kisha hapo. Ikiwa tulionana naye kwa mara ya kwanza Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, na anatumika muda wote wa juma, labda atataka tumrudilie tena Siku ya Posho ao Siku ya Yenga ya juma lifuatalo. Tunapopatana na mutu kwamba tutamrudilia siku fulani, tusikose kutimiza ahadi yetu.—Mt. 5:37.
5. Namna gani kuwarudilia watu bila kukawia kunatusaidia kutimiza kazi ya kufanya wanafunzi ambayo Yesu alituachia?
5 Tuna sababu nzuri za kuwarudilia haraka iwezekanavyo wale wenye kupendezwa. Kwa hiyo, tufanye mpango wa kuwarudilia bila kukawia, kwa kuwa “wakati uliobaki umepungua.” (1 Kor. 7:29) Kadiri tunavyojikaza kuwarudilia bila kukawia wenye kupendezwa na ujumbe wa Ufalme, ndivyo tutakavyopata matokeo mazuri.