Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/10 uku. 1
  • “Usiogope”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Usiogope”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kujua Kama Yehova Anatupenda Kunatusaidia Tupiganishe Woga
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Yehova Atakutia Nguvu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Piganisha Woga kwa Kumutegemea Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • “Usihangaike, kwa Maana Niko Mungu Wako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 10/10 uku. 1

“Usiogope”

1. Ni matatizo gani yanayofanana na yale ya Yeremia tunayoweza kupambana nayo leo?

1 Yeremia alipopewa mgawo wa kuwa nabii, aliona kuwa hastahili. Lakini Yehova alimuhakikishia hivi, “usiogope,” na kwa fazili akamutia nguvu ili kutimiza mgawo wake. (Yer. 1:6-10) Katika siku zetu, kusikia haya ao mutu kufikiri kwamba hastahili kunaweza kufanya tusihubiri kama inavyofaa. Nyakati fulani, kuogopa jinsi watu watakavyoitikia ao maoni watakayokuwa nayo juu yetu kunaweza kutuzuia tusihubiri. Namna gani tunaweza kushinda woga huo, na hilo litatuletea baraka gani?

2. Namna gani kujitayarisha kutatusaidia tuondoe woga katika mahubiri?

2 Kujitayarisha Kimbele: Kujitayarisha vizuri kunaweza kutusaidia tusiogope. Kwa mfano, ikiwa tunatayarisha kimbele jinsi ya kushinda vizuia-mazungumzo, tutakuwa tayari kushinda vipingamizi vinavyotokea kwa ukawaida. (Met. 15:28) Kwa nini musitumie vipindi vya mazoezi wakati wa Ibada ya Familia ili kujitayarisha kuhusiana na vipingamizi vinavyoweza kutokea kwenye masomo na katika mahubiri?​—1 Pet. 3:15.

3. Namna gani kumtegemea Yehova kunatusaidia tushinde woga?

3 Kumtegemea Yehova: Kumtegemea Yehova kutatusaidia tusiwe na woga. Yehova anatuhakikishia kwamba atatusaidia. (Isa. 41:10-13) Huo ni ulinzi mkubwa kabisa. Zaidi ya hilo, Yesu alituhakikishia kwamba hata wakati tunapatwa na hali zisizotazamiwa, roho takatifu ya Mungu itatusaidia tutoe ushahidi kwa njia nzuri. (Marko 13:11) Kwa hiyo, umuombe Yehova roho yake takatifu kwa ukawaida.​—Luka 11:13.

4. Kuendelea kuhubiri ijapokuwa vipingamizi kunaleta baraka gani?

4 Baraka: Tunapovumilia katika kazi ya kuhubiri ijapokuwa matatizo, tunatiwa nguvu ili kupambana na majaribu ya wakati ujao na kuyashinda. Tunasitawisha bidii na ujasiri​—ambazo ni sifa za wale wanaojazwa roho takatifu. (Mdo. 4:31) Zaidi ya hilo, tunaposhinda woga kwa msaada wa Yehova, tunatia nguvu imani yetu na tunategemea mkono wake unaookoa. (Isa. 33:2) Pia tunapata furaha na tunatosheka kwa kuwa tunajua kwamba tunafurahisha Baba wetu wa mbinguni. (1 Pet. 4:13, 14) Acheni basi tusiogope na tuendelee kutangaza ujumbe wa Ufalme kwa ujasiri, tukiwa hakika sikuzote kwamba Yehova atatusaidia!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine