Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/11 uku. 2
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuwasaidie ‘Wasimame Katika Imani Bila Kutikisika’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna Kutaniko Linaweza Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 4/11 uku. 2

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Tunapaswa kujifunza na mwanafunzi wa Biblia mwenye kufanya maendeleo mpaka wakati gani?

Ni vizuri zaidi kuendelea kujifunza na mwanafunzi wa Biblia anayefanya maendeleo mpaka wakati atakapomaliza vitabu viwili, yaani Biblia Inafundisha Nini Hasa? na “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu.” Tutafanya hivyo hata ikiwa mwanafunzi anabatizwa mbele ya kumaliza vitabu hivyo viwili. Hata akiisha kubatizwa tunaweza kuendelea kuripoti saa, ziara za kurudia, na funzo. Ikiwa mhubiri fulani anatusindikiza na anashiriki katika funzo, yeye pia anaweza kuhesabu saa.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 3, 2009, ukurasa wa 2.

Ni jambo la maana wapya wapate msingi mzuri katika kweli mbele ya kuacha kujifunza nao. Wanapaswa kuwa ‘wametia mizizi’ katika Kristo na “kuimarishwa katika imani” ili washinde matatizo ambayo yatawapata. (Kol. 2:6, 7; 2 Tim. 3:12; 1 Pet. 5:8, 9) Zaidi ya hiyo, ili wafundishe watu wengine vizuri, wanapaswa kuwa na “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Kwa kujifunza nao mpaka kumaliza vitabu hivyo viwili, tunawasaidia watembee vizuri kwenye “barabara inayoongoza kwenye uzima.”—Mt. 7:14.

Mbele ya kukubali mutu abatizwe, wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba anaelewa vizuri mafundisho ya msingi ya Biblia na anaishi kulingana na mafundisho hayo. Wazee wanapaswa kuwa waangalifu hasa wanapomchunguza mwanafunzi ambaye hajamaliza kitabu cha kwanza cha funzo. Ikiwa mutu hayuko tayari kwa ajili ya ubatizo, wazee watahakikisha kwamba anatolewa msaada wa pekee utakaomsaidia atimize mambo yanayoombwa ili kubatizwa wakati ujao.—Ona kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 217-218.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 2]

Ni jambo la maana wapya wapate msingi mzuri katika kweli

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine