Tuwasaidie ‘Wasimame Katika Imani Bila Kutikisika’
Inafurahisha sana kuona namna Yehova anabariki kazi ya kukusanya watu. Kila mwaka, watu zaidi ya 250 000 wanabatizwa. (Kum. 28:2) Wahubiri wengi wana tabia ya kuacha kujifunza na mutu fulani kisha tu yeye kubatizwa; na wanaanza kuhangaikia kujifunza na watu wengine. Vilevile, wanafunzi nao kisha tu kubatizwa, wanaacha kujifunza ili wakuwe na wakati mwingi wa kuhubiri. Lakini, ni lazima wanafunzi wa Biblia wasimame katika kweli bila kutikisika. Wanapaswa kuwa na mizizi katika Kristo na kusimama katika imani bila kutikisika. (Kol. 2:6, 7; 2 Tim. 3:12) Kwa hiyo, kisha kubatizwa, mwanafunzi anapaswa kuendelea kujifunza mupaka amalize kitabu Biblia Inafundisha na kitabu “Upendo wa Mungu.”—Soma Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 4, 2011, ukurasa wa 2.