Nafasi za Zaidi za Kumusifu Yehova
1. Ni mupango gani mupya unaotutolea nafasi ya ‘kumusifu sana Yehova’?
1 Mwezi wa 3 uliopita, mupango mupya ulianza; mupango huo unawatolea wahubiri nafasi ya kuwa mapainia wasaidizi wa saa 30 katika Mwezi wa 3 na wa 4 kila mwaka, na katika mwezi ambamo mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko. Ikiwa juma la ziara linaanza mwishoni mwa mwezi mumoja na linamalizika mwanzoni mwa mwezi mwingine, muhubiri anaweza kuchagua mwezi mumoja ili kufanya upainia musaidizi wa saa 30. Mapainia wasaidizi wote watahuzuria mwanzo mupaka mwisho mukutano wa mwangalizi pamoja na mapainia wa kawaida na wa pekee. Hilo linamaanisha kwamba, hata ikiwa hatuna uwezo wa kuhubiri saa 50, tunaweza ‘kumusifu sana Yehova’ kama mapainia wasaidizi wa saa 30 mara ine kwa mwaka!—Zab. 109:30; 119:171.
2. Ndugu na dada watakaokuwa mapainia wasaidizi wakati mwangalizi atatembelea kutaniko watafaidika na nini?
2 Mwangalizi wa Muzunguko Anapotembelea Kutaniko: Sasa, wahubiri wengi zaidi wanaweza kuwa mapainia wasaidizi mwangalizi anapotembelea kutaniko na kufaidika na ubadilishanaji wa kitia-moyo wanapohubiri pamoja naye. (Rom. 1:11, 12) Mapainia wasaidizi wengi wanaweza kuomba pumuziko kwenye kazi ili kuhubiri pamoja naye katika juma. Wale ambao ni wafanya-kazi wanaweza kumuomba mwangalizi wahubiri pamoja naye Siku ya Posho ao Siku ya Yenga. Tena, itakuwa jambo lenye kutia moyo kabisa kwa mapainia wasaidizi kuhuzuria mukutano wa mwangalizi pamoja na mapainia wa kawaida na wa pekee!
3. Sababu gani Mwezi wa 3 na wa 4 ni miezi inayofaa zaidi ili kuwa painia musaidizi?
3 Katika Mwezi wa 3 na wa 4: Wale waliokuwa mapainia wasaidizi wa saa 30 mwezi mumoja katika kipindi cha Ukumbusho wanaweza kuzidisha ‘zabihu yao ya sifa’! (Ebr. 13:15) Mwezi wa 3 na wa 4 ni miezi inayofaa zaidi ili kupanua utumishi wetu kwa kufanya upainia musaidizi. Kila mwaka katika miezi hiyo, tunafanya kampanye ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho. Tena, kwa kuwa ndugu na dada wengi wanahubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho, tuna nafasi ya kuhubiri na wahubiri mbalimbali. Kisha Ukumbusho, tunafanya mupango wa kurudilia watu wenye kupendezwa waliohuzuria Ukumbusho na kuwatia moyo wahuzurie hotuba ya pekee. Je, moyo wako utakuchochea utumie nafasi hizo za pekee ili kuwa painia musaidizi?—Lu. 6:45.