Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 2
“Watu tunaozungumuza nao wana mawazo tofauti kuhusu Biblia. Wamoja wanaamini kwamba ni Neno la Mungu; wengine wanasema ni kitabu kama vitabu vingine. Wewe unawaza nini?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, na muzungumuzie habari ya chini ya ulizo la kwanza na musome hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/02
“Watu wengi wanataka vita iishe. Unawaza inawezekana amani ikuwe duniani pote? [Acha mutu ajibu.] Ona mambo ambayo maandiko yanasema. [Soma Zaburi 46:9.] Mambo yaliyotokea wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu yanatusadikisha kwamba karibuni Mungu atatimiza unabii huo na kumaliza vita. Gazeti hili linafasiria mambo hayo.”
Amuka! Mwezi wa 2
“Tunatembelea watu ili kuzungumuza nao kwa muda mufupi juu ya jambo fulani linalohangaisha watu wengi. Inaonekana hatuna wakati wa kutosha. Unawaza tunakosa wakati kwa sababu tuna mengi ya kufanya ao tunatumia wakati mubaya? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi hawajue kwamba Biblia inatutolea mashauri mazuri ya kutusaidia tutumie wakati wetu muzuri. Kwa mufano. [Soma Wafilipi 1:10a.] Gazeti hili linazungumuzia njia ine ambazo zimewasaidia watu wengi kutumia wakati wao kwa hekima.”