Mwaliko wa Pekee
1. Kampanye ya kuwaalika watu kwenye mikusanyiko yetu ya 2014 itaanza wakati gani?
1 Ikiwa unatayarisha chakula cha pekee kwa ajili ya marafiki ao watu wa familia, kinakuchukulia wakati na unatumia feza nyingi, ni kweli kwamba utakuwa mwenye furaha unapowaalika watu kwenye mulo. Vilevile, mambo mengi yamefanywa ili kutayarisha chakula cha kiroho ambacho kitatolewa kwenye mikusanyiko yetu ya wilaya na ya kimataifa ya 2014. Majuma matatu mbele mikusanyiko hiyo ianze, tutakuwa na pendeleo la kuwaalika watu ili waihuzuirie. Jambo gani litatusaidia kuwaalika watu kwa bidii?
2. Ni nini itatuchochea tushiriki kwa bidii katika kampanye?
2 Ikiwa tunafikiria sana namna tunavyofaidika na chakula cha kiroho ambacho Yehova anatutolea kwenye mikusanyiko yetu, tutachochewa kushiriki kwa bidii katika kampanye hiyo. (Isa. 65:13, 14) Tusisahau pia kwamba kampanye yetu ya kuwaalika watu kwenye mikusanyiko inakuwa na matokeo mazuri. Watu fulani kati ya wale tutakaoalika watafika kwenye mukusanyiko. Iwe watu watafika ao hapana, kufanya kampanye hiyo kwa bidii kutamuletea Yehova utukufu na kutaonyesha ukarimu wake.—Zab. 145:3, 7; Ufu. 22:17.
3. Tutawaalika watu namna gani?
3 Wazee watafanya mipango ili wahubiri wawatolee watu wengi zaidi mialiko, wataamua pia ikiwa wahubiri wanaweza kuacha mialiko kwenye nyumba ambazo hawakukuta watu ao hata kuitolea watu mahali pa watu wengi katika eneo lenu. Siku ya Posho na Siku ya Yenga magazeti yatatolewa pamoja na mialiko ikiwezekana. Ikiwa Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi inafika wakati kampanye ingali na endelea, kuliko kuanzisha mafunzo, tutawaalika watu. Kisha kampanye, tutakuwa wenye furaha sana kwa kujua kwamba tulishiriki kwa bidii katika kampanye na kwamba tuliwaalika watu wengi sana kwenye chakula cha kiroho ambacho Yehova ametutayarishia.
[Sanduku katika ukurasa wa 4]
Tutasema Nini?
Kisha kumusalimia mutu, unaweza kusema: “Duniani pote, tunawaalika watu kwenye tukio la maana sana. Mahali, siku, na saa vimeandikwa kwenye mwaliko.”