Usikawie Kumualika Mutu
1. Kampanye ya kuwaalika watu kwenye mukusanyiko wetu wa eneo itaanza wakati gani?
1 Kama unatayarisha chakula fulani cha pekee kwa ajili ya familia ao marafiki na matayarisho hayo yanakuchukulia wakati na feza nyingi, kwa kweli utakuwa mwenye furaha wakati unawaalika. Kwa njia hiyo, mambo mengi yamefanywa kwa ajili ya kutayarisha chakula cha kiroho chenye kitatolewa kwenye mukusanyiko wetu wa eneo wa mwaka huu. Majuma matatu mbele ya mukusanyiko wetu wa eneo kuanza, Yehova anatupatia pendeleo la kualika wengine kwenye mukusanyiko wetu. Ni nini itatusaidia kualika watu kwa furaha?
2. Ni nini itatusaidia kualika watu kwa furaha?
2 Tutakuwa na furaha ya kuwaalika watu wengi kama tunafikiri sana juu ya baraka yenye tulipata kwenye mikusanyiko ya eneo kupitia mafundisho yenye kutia moyo. (Isa. 65:13, 14) Tunapaswa pia kukumbuka kama kila mwaka kampanye yetu inaleta matokeo mazuri. (Ona kisanduku “Kampanye Yetu Ilileta Matokeo Mazuri.”) Watu fulani kati ya wenye tutaalika watakuja kwenye mukusanyiko wetu wa eneo na wengine hawatakuja. Hata kama hatujue ni watu ngapi watakuja, tujue kama tukijikaza kualika watu wengi sana wakati wa kampanye tutamuletea Yehova utukufu na tutaiga roho yake ya kutoa.—Zab. 145:3, 7; Ufu. 22:17.
3. Namna gani tutawatolea watu mialiko?
3 Kila baraza la wazee litachukua mipango ili wahubiri waachie watu wengi sana mialiko. Wazee wataamua pia kama ni muzuri kutoacha mialiko chini ya milango ya watu wenye hawatakuwa kwao ili mialiko hiyo itolewe kwa kuhubiri mahali pa watu wengi katika eneo. Siku ya Posho na Siku ya Yenga, magazeti yatatolewa pamoja na mialiko kama inawezekana. Kwenye mwisho wa kampanye, tutakuwa wenye furaha sana kujua kama tulifanya yetu yote ili kuwaalika watu wengi sana kwenye karamu ya kiroho yenye Yehova alitutayarishia.