Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/15 uku. 4
  • Usikawie Kumualika Mutu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usikawie Kumualika Mutu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mwaliko wa Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kampanye Yenye Matokeo Mazuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Kampanye ya Kualika Watu Kwenye Mukusanyiko wa Eneo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Kampanye ya Kugawia Watu Mialiko ya Ukumbusho Itaanza Tarehe 2 Mwezi wa 4
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 4/15 uku. 4

Usikawie Kumualika Mutu

1. Kampanye ya kuwaalika watu kwenye mukusanyiko wetu wa eneo itaanza wakati gani?

1 Kama unatayarisha chakula fulani cha pekee kwa ajili ya familia ao marafiki na matayarisho hayo yanakuchukulia wakati na feza nyingi, kwa kweli utakuwa mwenye furaha wakati unawaalika. Kwa njia hiyo, mambo mengi yamefanywa kwa ajili ya kutayarisha chakula cha kiroho chenye kitatolewa kwenye mukusanyiko wetu wa eneo wa mwaka huu. Majuma matatu mbele ya mukusanyiko wetu wa eneo kuanza, Yehova anatupatia pendeleo la kualika wengine kwenye mukusanyiko wetu. Ni nini itatusaidia kualika watu kwa furaha?

2. Ni nini itatusaidia kualika watu kwa furaha?

2 Tutakuwa na furaha ya kuwaalika watu wengi kama tunafikiri sana juu ya baraka yenye tulipata kwenye mikusanyiko ya eneo kupitia mafundisho yenye kutia moyo. (Isa. 65:13, 14) Tunapaswa pia kukumbuka kama kila mwaka kampanye yetu inaleta matokeo mazuri. (Ona kisanduku “Kampanye Yetu Ilileta Matokeo Mazuri.”) Watu fulani kati ya wenye tutaalika watakuja kwenye mukusanyiko wetu wa eneo na wengine hawatakuja. Hata kama hatujue ni watu ngapi watakuja, tujue kama tukijikaza kualika watu wengi sana wakati wa kampanye tutamuletea Yehova utukufu na tutaiga roho yake ya kutoa.—Zab. 145:3, 7; Ufu. 22:17.

3. Namna gani tutawatolea watu mialiko?

3 Kila baraza la wazee litachukua mipango ili wahubiri waachie watu wengi sana mialiko. Wazee wataamua pia kama ni muzuri kutoacha mialiko chini ya milango ya watu wenye hawatakuwa kwao ili mialiko hiyo itolewe kwa kuhubiri mahali pa watu wengi katika eneo. Siku ya Posho na Siku ya Yenga, magazeti yatatolewa pamoja na mialiko kama inawezekana. Kwenye mwisho wa kampanye, tutakuwa wenye furaha sana kujua kama tulifanya yetu yote ili kuwaalika watu wengi sana kwenye karamu ya kiroho yenye Yehova alitutayarishia.

Utasema Nini?

Kisha kumusalimia mutu, unaweza kusema hivi: “Katika dunia yote tunawatolea watu mualiko huu kwa ajili ya tukio la maana sana. Tarehe, saa na mahali pa kufanyia tukio hilo vinapatikana kwenye mualiko.”

Kampanye Yetu Ilileta Matokeo Mazuri

  • Kumepita miaka mingi, dada mumoja alikuwa katika kampanye ya kuwaalika watu na alikuwa akijiuliza kama kampanye hiyo italeta kabisa matokeo mazuri. Alijiuliza hivi: ‘Watu wataitika kabisa kukuja kwenye mukusanyiko wetu wa eneo?’ Asubui ya Siku ya Posho, aliona pembeni yake mwanaume mumoja wa dini ya Sikh na aliamua kujitambulisha kwake. Mwanaume huyo alimuambia kwamba alikuja kwenye mukusanyiko wetu wa eneo kwa sababu alipata mualiko. Aliuliza maulizo mengi na dada aliweza kumujibu. Alisema kwamba alifurahia sana mafundisho na alivutiwa na mwenendo na mavazi ya watu wenye walikuja kwenye mukusanyiko. Siku hiyo hiyo, dada huyo alianzisha mazungumuzo na bibi na bwana wenye kukaa pempeni yake. Wao pia walisema kwamba walipokea mualiko na wakachukua motokari ya watu wengi ili kuja kwenye mukusanyiko. Walifurahia mukusanyiko na waliamua kukuja tena Siku ya Yenga. Mambo hayo yalifanya dada huyo atambue kwamba ni jambo la maana sana kufanya kampanye kila mwaka.

  • Kwenye mukusanyiko wa eneo wa hivi karibuni, bibi na bwana mapainia wa kawaida walijitambulisha kwa bibi na bwana wenye kuzeeka. Bibi na bwana hao wenye kuzeeka walisema kwamba ilikuwa mara yao ya kwanza kufika kwenye mukusanyiko wa eneo. Mapainia waliwauliza: “Ni nani aliwaalika?” Walijibu: “Tulikuta mualiko chini ya mulango wetu”. Walisoma mualiko huo na kujaza sehemu yake ya nyuma. Ndugu na dada wengine waliwaalika kwenye chakula chao cha muchana. Walifurahia sana mukusanyiko na walipanga kuja tena siku yenye kufuata. Mipango ilikamatwa ili kuwatembelea.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine