Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/13 uku. 5
  • Kampanye Yenye Matokeo Mazuri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kampanye Yenye Matokeo Mazuri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Usikawie Kumualika Mutu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Kampanye ya Kualika Watu Kwenye Mukusanyiko wa Eneo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Mwaliko wa Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Tujikaze Sote Pamoja Ili Kutangazia Watu Ulimwenguni Pote Mkusanyiko wa Wilaya “Mfuate Kristo!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 4/13 uku. 5

Kampanye Yenye Matokeo Mazuri

Majuma matatu mbele ya mukusanyiko wa wilaya, makutaniko yatafanya tena kampanye ya kuwaalika watu wa eneo lao wanaopendezwa ili waje kuhuzuria. Kuna sababu nzuri ya kufanya kampanye hiyo ya kila mwaka. Mara nyingi wale wanaokubali mwaliko na kufika kwenye mukusanyiko wanashangazwa na hotuba zinazotegemea Biblia, biro mbalimbali zinazopangwa vizuri na watu waliojitolea, mwenendo muzuri, na umoja wetu. (Zab. 110:3; 133:1; Isa. 65:13, 14) Lakini, je, kampanye tunayofanya inakuwa na matokeo mazuri, zaidi sana katika maeneo ambamo watu wanaopendezwa wanapaswa kufanya safari ndefu ili kuhuzuria mukusanyiko?

Kisha mukusanyiko wa wilaya wa 2011, biro moja ya tawi ilipokea barua ya mwanamuke aliyepata mwaliko chini ya mulango wake. Sikuzote alijificha wakati Mashahidi wa Yehova waligonga kwenye mulango wake. Aliandika hivi: “Nilikuwa na nyumba nzuri, bwana muzuri, na nilifikiri kwamba nilikuwa na kila kitu ninachohitaji ili kuwa mwenye furaha. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, sikupata furaha, na kwa kweli maisha yangu hayakuwa na kusudi. Kwa hiyo, niliamua kusafiri kilometre 320 ili kuhuzuria programe ya Siku ya Posho.” Alifurahia sana mukusanyiko, kwa hiyo akamuita bwana yake ili kumuambia kwamba atabaki ili kuhuzuria pia programe ya Siku ya Yenga. “Nilisikiliza hotuba zote, nilikutana na Mashahidi wa Yehova wengi, na nilitaka mukusanyiko uendelee.” Aliporudi nyumbani, alianza kujifunza na kisha miezi ine akakuwa muhubiri asiyebatizwa. “Ninafurahi sana kwa kuwa nilipata mwaliko huo chini ya mulango wangu kwa sababu sasa maisha yangu ni yenye kusudi kabisa!”

Watu fulani wanaopokea mwaliko watahuzuria mukusanyiko. Kwa hiyo, shiriki kwa bidii katika kampanye hiyo ya maana. Mialiko itakayobaki, uipeleke katika muji ambamo mukusanyiko utafanywa, na uitumie ili kuhubiri wakati haukupanga kufanya hivyo.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Namna ya Kumutolea Mutu Mwaliko

Ili kuwatolea watu wengi wa eneo letu mialiko, ni vizuri tusiseme mambo mengi. Tunaweza kusema hivi: “Jambo. Duniani pote tunagawia watu mwaliko huu. Kamata mwaliko wako. Utapata maelezo mengine katika mwaliko.” Useme kwa uchangamufu. Tunaposhiriki katika kampanye Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, tuwatolee watu magazeti pia ikiwa inawezekana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine