Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/14 uku. 4-5
  • ‘Endelea Kuwa na Mwenendo Muzuri Kati ya Watu’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Endelea Kuwa na Mwenendo Muzuri Kati ya Watu’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mukusanyiko wa Eneo wa 2015
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Mwenendo Unaomutukuza Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Mikusanyiko Yetu ya Wilaya—Inashuhudia Kabisa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 4/14 uku. 4-5

‘Endelea Kuwa na Mwenendo Muzuri Kati ya Watu’

1. Sababu gani ni lazima tuendelee kuwa na mwenendo muzuri wakati wa mukusanyiko wa wilaya unaokuja?

1 Kila mwaka, wakati wa mikusanyiko yetu ya wilaya, watu wanatutazama. Kwa hiyo, kupitia mwenendo wetu, ni lazima tuonyeshe kabisa kwamba sisi ni waabudu wa Mungu. (Law. 20:26) Tabia yetu nzuri, namna yetu ya kuvaa na kujipamba vinapashwa kututambulisha kabisa kuwa Wakristo wa kweli. Tutakapohuzuria mikusanyiko yetu ya wilaya ao ya kimataifa, namna gani tunaweza ‘kuendelea kuwa na mwenendo muzuri kati ya watu,’ na kwa hiyo, kumuletea Baba yetu wa mbinguni utukufu?​—1 Pet. 2:12.

2. Tutaonyesha sifa gani za kikristo wakati wa mukusanyiko wetu wa wilaya?

2 Onyesha Sifa za Kikristo: Namna tunavyoonyeshana upendo na namna tunavyowatendea ‘wale walio inje’ ni tofauti kabisa na ya watu wa ulimwengu. (Kol. 3:10; 4:5; 2 Tim. 3:1-5) Tunapashwa kuwa watu wazuri na kuwavumilia wafanyakazi kwenye hoteli na kwenye restora, hata kama hatuelewane nao. Tabia nzuri itatuchochea pia tuwapatie zawadi watu wanaotufanyia kazi fulani ikiwa ni desturi kwenu.

3. Wazazi wanakumbushwa nini, na kwa sababu gani?

3 Wazazi wanapashwa kuwachunga watoto wao wanapokuwa kwenye mukusanyiko, kwenye restora, na kwenye hoteli. (Met. 29:15) Musimamizi mumoja wa hoteli alimuambia ndugu fulani na bibi yake hivi: “Tunawapenda Mashahidi wa Yehova. Ninyi na watoto wenu muko watu wazuri na muna adabu. Wafanya​-kazi wote wanawasifu, na tungependa muwe na kuja kila juma.”

4. Tutakapokuwa katika muji ambamo mukusanyiko utafanywa, tunapashwa kuvaa na kujipamba namna gani?

4 Vaa Muzuri: Wakati wa mukusanyiko tunapashwa kuvaa mavazi yanayofaa na yenye kiasi, tusivae kama watu wa Ulimwengu. (1 Tim. 2:9) Tunapofika kwenye hoteli ao tunapoondoka, na hata wakati wa kujifurahisha mbele na kisha mukusanyiko, tusivae ovyo​-ovyo. Kwa hiyo, tutajisikia huru kuvaa kadi ya kututambulisha na kuwa tayari kutoa ushahidi wakati nafasi inajitokeza. Ikiwa tunavaa na kujipamba kwa njia inayofaa, na tunakuwa na mwenendo muzuri wakati wa mukusanyiko wetu wa wilaya wa 2014, watu wenye kufuatia haki watavutiwa na habari ya Biblia yenye kuokoa uzima. Yehova pia atafurahi.​—Sef. 3:17.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Mukusanyiko wa Wilaya 2014​—Mambo ya Kukumbuka

◼ Saa: Siku zote tatu programu itaanza asubuhi pa saa 2:00 (8:00). Lakini, katika miji mikubwa​-mikubwa kama vile: Bandundu-Ville, Boma, Brazzaville, Bumba, Goma, Kananga, Kikwit, Kinshasa, Kisangani, Kolwezi, Likasi, Lodja, Lubumbashi, Matadi, Mbandaka, Mbuji Mayi, Mwene Ditu, Pointe Noire na Tshikapa, programu itaanza kila siku asubuhi pa saa 3:20 (9:20). Siku zote tatu muziki wa kufungua utaanza asubuhi pa saa moja ao saa mbili ya asubuhi kulingana na mahali. Wakati huo, sisi wote tunapashwa kukaa ili programu iweze kuanza kwa utaratibu. Programu itamalizika pa saa 9:55 (15:55) Siku ya Tano na Siku ya Posho, pa saa 8:40 (14:40) Siku ya Yenga. Itamalizika saa moja baadaye katika miji mikubwa​-mikubwa inayotajwa hapo juu.

◼ Kuchungia Wengine Viti: Munaweza kuchungia viti wale tu munaoishi nao, wale munaosafiri nao katika motokari moja ao wale munaojifunza nao Biblia.

◼ Chakula cha Midi: Inapendekezwa kwamba kila mutu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, kwa mufano: mikate ao keki, matunda, kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa ao chai vinapashwa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwe kuleta pombe kwenye mukusanyiko. Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa wauzishaji hao kunasaidia kuonyesha kama sisi ni watu safi. (Tafazali, Mujue kama wale wanaouzisha chakula inje hawaruhusiwe kuingia katika eneo la mukusanyiko wakati wowote.​—Yoh. 2:13-17).

◼ Usafi: Imeonekana mara nyingi kwamba wale wanaonunua chakula inje wanatupa chini makaratasi ao plastiki. Kwa hiyo, uwanja wote unajaa makaratasi, plastiki, machupa, na kazalika. Ikiwa mutu anaamua kununua chakula inje (kwa mufano bombo, biskwiti, ndazi ao vitumbua, samaki ao chakula kingine) anapashwa kutupa makaratasi ya kufungia vyakula katika kitunga cha uchafu kuliko kuyatupa chini. Tukiona mutu fulani ametupa chini kipande cha karatasi ao cha plastiki, tunapashwa kukiokota na kukitupa katika kitunga cha uchafu. Tafazali, tujikaze sana ili kulinda mahali petu pa mukusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kila mutu anayehuzuria anapashwa kulinda usafi. Ikiwa kila mumoja wetu anatimiza sehemu yake, mwishoni mwa kila siku, mahali pa mukusanyiko patabaki safi. Tunapenda kuonyesha katika maisha yetu sifa za Mungu mutakatifu ambaye tunaabudu.​—1 Pet 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.

◼ Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mukusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea mahali pa mukusanyiko, ili kutegemeza kazi ya duniani pote. Sheke zote zinazotolewa kwenye mukusanyiko zinapashwa kuandikwa kwa jina “Association ‘Les Témoins de Jéhovah.’”

◼ Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda kwa Uharaka: Ikiwa kwenye mukusanyiko kunatokea jambo fulani linaloomba kutenda kwa uharaka, tafazali unaweza kumuelezea ndugu mukaribishaji aliye karibu ambaye, bila kuchelewa, atajulisha ndugu wanaoshugulika na Matunzo ya Haraka ili waamue ikiwa hali inaomba kutoa musaada unaohitajiwa.

◼ Dawa: Ikiwa unatumia dawa ulizoagizwa na daktari, tafazali usisahau kubeba dawa zako kwa kuwa hazitapatikana mahali pa mukusanyiko. Kwa kuwa shindano za wale wanaogonjwa diabete ni zenye hatari, zinapashwa kutupwa mahali panapofaa; hazipashwe kutupwa katika chombo cha kutupia uchafu.

◼ Kukamata Picha: Ikiwa unataka kukamata picha wakati wa mukusanyiko, tafazali usitumie mwangaza (flash). Tafazali, usiwaite wale wanaofanya kazi ya kukamata picha mahali pa mukusanyiko. Ikiwa unawaona wakitafuta mutu wa kukamata picha, usikubali wakukamate picha.​—Yoh 2:13-17.

◼ Fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43): Wakati wa mukusanyiko, ikiwa unakutana mutu na anapendezwa, unapashwa kutumia fomu Tafadhali Fuatia Upendezi ili kutoa habari juu ya mutu huyo. Unaweza kuwaachia ndugu kwenye Idara ya Vitabu fomu ulizojaza ili zishugulikiwe, ao umupe mwandishi wa kutaniko lenu.

◼ Restora: Unapokuwa kwenye restora, fanya jina la Yehova liheshimiwe kupitia mwenendo wako muzuri. Vaa kwa njia inayofaa kwa Wakristo. Ikiwa ni kawaida kwenu kumupatia mufanyakazi wa restora matabishi kidogo, unaweza kumupatia.

◼ Mahali Tunapangishwa:

(1) Tafazali usiwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba kuliko inavyoruhusiwa ao kukubaliwa na mutu aliyekupangisha kwake. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la kupangishwa, fanya hivyo bila kukawia. (3) Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba ao ndugu wanaoshugulika na upangishaji kwenye Jumba la Ufalme ile ujue kile kinachohitajiwa ili kuepuka hatari yoyote. (4) Usipitishe kiasi unapotumia vitu vyovyote vinavyotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, pakiwa safi. Hilo linahusu pia Jumba la Ufalme, ambalo linaweza kutumiwa kuwa mahali pa kupangisha ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha tunda la roho unaposhugulika na wengine, iwe ni mwenye nyumba ao ndugu wengine Wakristo ambao labda munapangishwa pamoja nao.​—Gal. 5:22, 23.

◼ Kazi ya Kujitolea: Yeyote anayetaka kufanya kazi anapashwa kujulisha Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea Kufanya Kazi kwenye mukusanyiko. Watoto walio na miaka chini ya 16 wanaweza kutumika chini ya uongozi wa muzazi ao mutu aliyewaleta ao mutu mwingine mwenye kukomaa aliyekabiziwa watoto hao na muzazi.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Barua Kutoka Baraza Linaloongoza

Watumishi Wenzetu Wapendwa:

Tunafurahi sana kuwaandikia mwanzoni mwa mwaka huu wa pekee! Kukaribia mwisho wa mwaka wa 2014, kutakuwa kumepita miaka 100 tangu Yesu Kristo, Mufalme wetu mupendwa, aanze kutawala katikati ya maadui wake.​—Zab. 110:1, 2.

Mwanzoni mwa mwaka huu wa utumishi, kwenye mukutano wa kila mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, Halmashauri ya kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya ilitangaza kutolewa kwa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa katika Kiingereza; Biblia hiyo ndiyo tafsiri nzuri zaidi inayoweza kupatikana. Yehova alitumia wana wake waliozaliwa kwa roho ili watoe Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa. (Rom. 8:15, 16) Kwa kweli, jambo hilo ndilo linafanya tafsiri hiyo iwe ya pekee, sivyo?

Kwa muda wa miaka mingi, Halmashauri ya Uandikaji ya Baraza Linaloongoza imetia jambo la kutafsiri Biblia pa nafasi ya kwanza. Leo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inapatikana katika luga 121, yote nzima ao kwa sehemu. Tunawatia moyo mumuonyeshe Yehova kwamba munapendezwa sana na Biblia hiyo. Muisome na kuitafakari kila siku. Kwa kufanya hivyo, mutamukaribia zaidi Yehova Mungu, Mutungaji wayo.​—Yak. 4:8.

Tunahuzunika wakati tunasikia kwamba ndugu na dada zetu wapendwa wanapata majaribu. Kwa kweli, wakati fulani inaweza kuwa vigumu kwao kufurahi pamoja na ndugu zao. Kwa mufano, siku zilizopita, maisha ya familia moja katika Asia ilivurugika sana wakati mama wa familia hiyo alipatwa na ugonjwa wa kupooza bila kutazamia. Jambo lenye kuhuzunisha ni kwamba waganga wenye uzoefu hawakuweza kumuponyesha! Bwana yake analazimika kumushugulikia kila wakati. Mwana wao na binti zao wawili wanaonyesha kwamba wao ni Wakristo wa kweli kwa kuwasaidia wazazi wao kwa upendo. Familia hii na ninyi wote ambao mumepambana kwa uaminifu na majaribu mbalimbali munaweza kupata furaha inayotokana na kuvumilia majaribu. (Yak. 1:2-4) Iwe sisi ni watiwa​-mafuta ao wa kondoo wengine, Yehova anatuhakikishia kwamba tutakuwa wenye furaha kwa kuvumilia majaribu kwa kuwa tutapata zawadi ya uzima wa milele!​—Yak. 1:12.

Mwaka jana, watu 19 241 252 walihuzuria Ukumbusho. Inatia moyo sana kuona watu wengi zaidi wakimutukuza Yehova na Yesu Kristo kwa kuhuzuria mukutano wa maana zaidi wa watu wa Mungu katika mwaka! Ilifurahisha kabisa kuona watu wengi zaidi wakimutukuza Yehova kwa kuwa mapainia wasaidizi katika kipindi cha ukumbusho, katika Mwezi wa 3 na wa 4! Bila shaka ulifurahi wakati ulisikia kwamba wale wanaokuwa mapainia wasaidizi wakati mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko watahuzuria mwanzo mupaka mwisho mukutano wa mwangalizi pamoja na mapainia, hata kama mwangalizi anatembelea kutaniko katika miezi mingine tofauti na Mwezi wa 3 na wa 4! Watu wa kiroho wanaelewa kwamba ni lazima kuwa na bidii katika mahubiri na katika kazi za kutaniko. Kuwa na mengi ya kufanya kunatusaidia tubaki imara na bila kutikisika ili Ibilisi asizoofishe imani yetu na kutupotosha.​—1 Kor. 15:58.

Inatia moyo kuona kwamba katika mwaka wa utumishi uliopita watu 277 344 walijitoa kwa Yehova na kubatizwa katika maji, na sasa wako katika barabara inayoongoza kwenye uzima pamoja na ndugu zao wa ulimwenguni pote! (Mt. 7:13, 14) Ni lazima tuwategemeze wapya hao ili ‘wasimame katika imani’ (Kol. 2:7) Tuendelee basi kutiana moyo ili tuvumilie mupaka mwisho. (Mt. 24:13) ‘Muwaonye wale wasio na utaratibu, museme kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika, mutegemeze walio zaifu, muwe wenye ustahimilivu kuelekea wote.’ (1 Thes. 5:14) Kwa kumaliza, kila mumoja wetu ‘asali bila kuacha,’ akisema: ‘Ufalme wako uje.’​—1 Thes. 5:17; Mt. 6:10.

Tafazali, musome hicho Kitabu cha Mwaka na mujue kwamba tunapenda kila mumoja wenu kwa sababu munamupenda Yehova!

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine