Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/15 uku. 5-7
  • Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mukusanyiko wa Eneo wa 2015

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mukusanyiko wa Eneo wa 2015
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Endelea Kuwa na Mwenendo Muzuri Kati ya Watu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Mwenendo Unaomutukuza Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Mikusanyiko Yetu ya Wilaya—Inashuhudia Kabisa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 4/15 uku. 5-7

Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mukusanyiko wa Eneo wa 2015

  • Saa: Kila siku, programu itaanza na saa 2:20 (8:20). Lakini, programu itaanza kila siku na saa 3:20 (9:20) katika miji mikubwa-mikubwa hii: Bandundu-Ville, Boma, Brazzaville, Bumba, Goma, Kananga, Kikwit, Kinshasa, Kisangani, Kolwezi, Likasi, Lodja, Lubumbashi, Matadi, Mbandaka, Mbuji Mayi, Mwene Ditu, Pointe Noire na Tshikapa. Milango itafunguliwa na saa 1:00 (7:00) ao 2:00 (8:00) kulingana na muji. Wakati muziki unaanza, kila mutu anapaswa kamata nafasi yake ili programu ianze kwa utaratibu. Siku ya Tano na Siku ya Posho, programu itamalizika na saa 9:55 (15:55) na Siku ya Yenga, programu itamalizika na 8:40 (14:40). Lakini, katika miji yenye tulitaja hapo juu programu itamalizika saa moja kisha.

  • ‘Tumusifu Yehova kwa Wimbo’: Watu wa Mungu wa wakati wa zamani walimusifu Yehova kwa wimbo. Hata leo, muziki ni sehemu ya maana sana ya ibada ya kweli. (Zab. 28:7) Kila sehemu ya programu ya mukusanyiko wetu wa eneo inaanza na muziki wa sauti ya chini. Muziki huo hauko wa kutuburudisha tu, lakini umetayarishwa ili kutufundisha na kumusifu Yehova. Kwa hiyo, wakati musimamizi wa programu anatangaza kwamba muziki unataka kuanza, huo ni wakati wa kunyamaza na kusikiliza muziki. Tukifanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunaona kazi ya kikundi cha wanamuziki cha Watchtower kuwa ya maana. Mara mbili kila mwaka, ndugu na dada hao wanajilipia wenyewe safari yao ili kuja Patterson, New York, kwa ajili ya kutunga muziki mutamu sana ili tufurahi. Kisha kusikiliza muziki kwa uangalifu, tunapaswa kumusifu Yehova kwa kuimba nyimbo zetu za Ufalme.

  • Kuchungia Wengine Viti: Munaweza kuchungia viti watu wenye munaishi nao katika nyumba moja ao wenye munasafiri nao katika motari moja ao wenye munajifunza nao Biblia kwa sasa.

  • Kuvaa kwa Heshima: Tunapaswa kuvaa manguo yenye kustahili na tusiige namna ya kuvaa ya watu wa ulimwengu. (1 Tim. 2:9) Hata wakati tuko kwenye hoteli ao inje ya hoteli, ao tena wakati tunajifurahisha mbele ao kisha mikusanyiko, hatupaswe kuvaa ovyoovyo. Tutafurahia kuvaa kadi yetu ya utambulisho na tusiogope kuhubiri wakati nafasi inajitokeza. Namna tunavaa, namna tunajipamba na namna tunajiendesha wakati wa mikusanyiko yetu inaweza kuwachochea watu wengine wafurahie ujumbe wa Biblia wenye kuokoa na inaweza pia kumusifu Mungu wetu Yehova.—Zef. 3:17.

  • Kutumia Vitu vya Kielektroniki: Wakati wa programu, kutia telefone yetu na vyombo vingine vya kielektroniki katika hali yenye haitasumbua wengine, kunaonyesha kwamba tunawaheshimia wengine. Kama tunatumia kamera, tablette ao chombo kingine cha kielektroniki, tunapaswa kuwafikiria wengine kwa kutowasumbua ao kutowazuia kuona jukwaa. Tunaheshimia pia wengine kwa kutoandika-andika ujumbe kupitia telefone ao vyombo vingine vya kielektroniki wakati wa programu. Tafazali musiwaalike wapiga-picha wa kulipwa (photographe professionnel) kwenye mukusanyiko. Kama munawaona kwenye mukusanyiko, tafazali musikubali wawapige picha.—Yoh. 2:13-17.

  • Chakula cha Midi: Ni muzuri kila mutu alete chakula fulani chepesi lakini cha kujenga mwili kama vile mikate ao keki, matunda, kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa (café) ao chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwi kuleta pombe kwenye mukusanyiko.Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa wauzishaji hao kunasaidia kuonyesha kama sisi ni watu safi. (Tafazali, Mujue kama wale wanaouzisha chakula inje hawaruhusiwe kuingia katika eneo la mukusanyiko wakati wowote.—Yoh. 2:13-17.)

  • Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mukusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea mahali pa mukusanyiko, ili kutegemeza kazi ya duniani pote.Sheke zote zinazotolewa kwenye mukusanyiko zinapaswa kuandikwa kwa jina “ Association ‘ Les Témoins de Jéhovah.’”

  • Dawa: Kama unatumia dawa yenye doktere alikuandikia, tafazali usisahau kubeba dawa yako kwa sababu haitapatikana kwenye mukusanyiko. Kwa kuwa shindano za watu wenye kugonjwa diabete ni zenye hatari, zinapaswa kutupwa mahali penye kufaa; hazipaswi kutupwa katika chombo cha kutupia uchafu kwenye mukusanyiko.

  • Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda kwa Haraka: Kama kwenye mukusanyiko kunatokea jambo lenye linaomba kutenda kwa haraka, tafazali unaweza kumuelezea ndugu mukaribishaji mwenye kuwa karibu ili ajulishe bila kuchelewa ndugu wenye kusimamia Matunzo ya Haraka kusudi waone jambo la kufanya.

  • Fomu Tafazali Fuatia Upendezi (S-43): Ukimuona mutu fulani mwenye kupendezwa wakati wa mukusanyiko, unapaswa kutumia fomu Tafazali Fuatia Upendezi ili kutoa habari juu ya mutu huyo. Wahubiri wanapaswa kuja na fomu moja ao mbili kwenye mukusanyiko. Unaweza kuwaachia ndugu kwenye Biro ya Vitabu fomu zenye ulijaza ili wazitume, ao uzipatie mwandishi wa kutaniko lenu.

  • Restora: Wakati uko kwenye restora, fanya jina la Yehova liheshimiwe kwa kuonyesha mwenendo muzuri na kwa kuvaa muzuri. Kama ni kawaida kwenu kupatia mufanyakazi wa restora matabishi kidogo, unaweza kufanya hivyo.

  • Mahali Kwenye Tunapangishwa:

    1. Usikuwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba kuliko inavyoruhusiwa ao kukubaliwa na mutu mwenye alikupangisha kwake.

    2. Kama hautaki tena kupangishwa, sema bila kukawia.

    3. Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba; kama ulipangishwa kwenye Jumba la Ufalme uliza ndugu wenye kusimamia Jumba la Ufalme.

    4. ) Usitumie ovyoovyo vitu vyenye vinatolewa kwa ajili ya wageni. Unapaswa kuwa na kiasi na kutumia akili nzuri.

    5. Kila siku, uache safi mahali penye unapangishwa. Kama ndugu na dada wenye walitoka mbali wanapangishwa katika Jumba la Ufalme, wanapaswa pia kuliacha safi kila siku.

    6. Onyesha tunda la roho kwa mwenye nyumba ao kwa ndugu na dada wenye munapangishwa nao.—Gal. 5:22, 23..

  • Kazi ya Kujitolea: Mwenye anataka kufanya kazi anapaswa kujulisha Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea Kufanya Kazi kwenye mukusanyiko. Watoto wa miaka chini ya 16 wanaweza kutumika kama wanaongozwa na wazazi wao ao na mutu mwenye alimuleta ao na mutu mwengine mukubwa mwenye alipewa ruhusa na wazazi wa watoto hao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine