Jizoeze Kuheshimu Wakati
1. Yehova anatuonyesha mufano gani kuhusu kuheshimu wakati?
1 Siku zote, Yehova anafanya mambo kwa wakati. Kwa mufano, anawatolea watumishi wake ‘musaada kwa wakati unaofaa.’ (Ebr. 4:16) Pia anawatolea ‘chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa.’ (Mt. 24:45) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kwamba siku ya hasira yake inayokuja ‘haitachelewa.’ (Hab. 2:3) Tunafaidika sana kwa sababu Yehova anaheshimu wakati. (Zab. 70:5) Hata hivyo, kwa kuwa sisi ni wanadamu wasiokamilika na tuna kazi nyingi za kufanya, inaweza kuwa vigumu kwetu kuheshimu wakati. Sababu gani tunapashwa kujizoeza kuheshimu wakati?
2. Sababu gani kuheshimu wakati kunamutukuza Yehova?
2 Katika siku hizi za mwisho, si rahisi kuheshimu wakati kwa sababu watu wengi ni wenye kujipenda wenyewe na wasiojizuia. (2 Tim. 3:1-3) Kwa hiyo, Wakristo wanapoheshimu wakati wa kazi, wakati waliopanga kuonana na mutu fulani, na wakati wa mikutano, watu wengine wanatambua jambo hilo na kumutukuza Yehova. (1 Pet. 2:12) Je, kila mara unaanza kazi yako ya kimwili kwa wakati, lakini unajikuta mara nyingi umechelewa wakati wa mambo ya kiteokrasi? Kufika kwa wakati kwenye mikutano ya Kikristo ni kufika mbele ya wimbo na sala; kufanya hivyo kunaonyesha kwamba tunatamani kumuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye mupango ao utaratibu.—1 Kor. 14:33, 40.
3. Sababu gani kufika kwa wakati kunaonyesha kwamba tunawaheshimu wengine?
3 Kuheshimu wakati kunaonyesha kwamba tunawaheshimu wengine. (Flp. 2:3, 4) Kwa mufano, tunapofika kwa wakati kwenye mikutano ya Kikristo, kutia ndani mikutano kwa ajili ya mahubiri, hatutawavuruga Wakristo wenzetu. Kwa upande mwengine, ikiwa tunazoea kuchelewa, wengine watawaza kwamba tunaona wakati yetu kuwa ya maana sana kuliko wakati yao. Kufika kwa wakati kunaonyesha kwamba sisi ni watu wenye kutumainika, wenye bidii na wanaochukua mambo kwa uzito—sifa ambazo watu wanaotuzunguka wanafurahia.
4. Ikiwa tunazoea kuchelewa, namna gani tunaweza kufanya mabadiliko?
4 Ikiwa unazoea kuchelewa, tafuta kujua ni sababu gani. Panga muzuri programu yako ili ikuruhusu kufanya kazi zako kwa wakati ambao ulipanga. (Mhu. 3:1; Flp. 1:10) Muombe Yehova akusaidie. (1 Yoh. 5:14) Kuheshimu wakati ni njia moja ya kuonyesha kwamba tunapendezwa na amri mbili za Sheria zilizo kubwa zaidi, ni kusema, kumupenda Mungu na jirani yetu.—Mt. 22:37-39.