Miaka Mia Moja ya Kutangaza Ufalme!
1. Watu wa Yehova walichochewa kufanya nini karibu miaka mia moja iliyopita?
1 “Mutazame, Mufalme anatawala! Ninyi ndio wajumbe wake. Kwa hiyo mutangaze, mutangaze, mutangaze, Mufalme na ufalme wake.” Maneno hayo yenye kuchochea sana ambayo Ndugu Rutherford alisema kumepita karibu miaka mia moja, yalichochea watu wa Yehova kuendelea kutangaza ujumbe wa Ufalme katika sehemu za mbali za dunia. Na ni vile tumefanya! Kama Wakristo wa kwanza-kwanza, tumehubiri habari njema ya Ufalme “katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu.” (Kol. 1:23) Tukichunguza miaka mia moja ambayo imepita, tumefanya nini ili kutangaza Ufalme wa Mungu? Namna gani tunaweza kuendelea kutangaza Ufalme wakati huu ambao tunakaribia miaka 100 tangu uanze kutawala?
2. Namna gani vichapo vyetu vimezungumuzia sana Ufalme wa Mungu?
2 Mambo Tuliyofanya Wakati Uliopita: Kwa miaka mingi, Vichapo vyetu vimezungumuzia sana Ufalme wa Mungu. Kuanzia mwaka wa 1939 gazeti letu la musingi limeitwa: Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Kila mara, gazeti hili linazungumuzia Ufalme na mambo ambayo utatimiza. Pia, Gazeti Amuka! linakazia kwamba Ufalme wa Mungu tu ndio tumaini kwa wanadamu. Ni jambo lenye kufaa kabisa kwamba magazeti hayo ndiyo yanachapishwa na kugawanywa sana kupita magazeti mengine yote katika dunia!—Ufu. 14:6.
3. Tumetumia njia gani mbalimbali ili kutangaza Ufalme?
3 Watu wa Yehova wametumia njia mbalimbali ili kutangaza Ufalme. Mwanzoni, tulitumia motokari zenye kuwa na vikuza sauti, vituo vya radio, na gramafoni ao fono za kubeba kwa mukono. Njia hizo zilitusaidia kutangaza habari njema kwa watu wengi zaidi wakati ambapo wahubiri wa Ufalme walikuwa wachache sana. (Zab. 19:4) Katika miaka ya hivi karibuni, tumetangaza habari kwenye adresi yetu ya Internete jw.org ili kuwahubiria watu wengi Ufalme—na hata wale walio katika maeneo ambayo kazi yetu inakatazwa.
4. Tumeanzisha programu gani za pekee ili kuhubiri?
4 Watu wa Yehova wameanzisha pia programu za pekee ili kutangaza ujumbe wa Ufalme. Kwa mufano, kuanzia mwaka wa 1995, zaidi ya mahubiri ya nyumba kwa nyumba, tumejikaza kuhubiri kwenye bustani za watu wote, mahali pa kuegeshea magari (ao parking), na mahali pa biashara. Hivi karibuni, tumeanzisha programu ya pekee ya kuhubiri mahali pa watu wengi katika miji mikubwa-mikubwa. Zaidi ya hayo, wahubiri wa makutaniko mengi wanahubiri mahali pa watu wengi katika eneo lao kwa kuweka vichapo kwenye meza ao kwenye vyombo vingine vya kusukuma. Lakini, tunaendelea kuona mahubiri ya nyumba kwa nyumba kuwa njia kubwa zaidi ya kuhubiri Ufalme.—Matendo 20:20.
5. Mwaka mupya wa utumishi utatolea wengi kati yetu nafasi ya kufanya nini?
5 Mambo ya Kufanya Wakati Unaokuja: Tunapoanza mwaka mupya wa utumishi katika Mwezi wa 9, wahubiri wengi watakuwa mapainia wa kawaida. Wewe pia utakuwa painia wa kawaida? Ikiwa haitawezekana, unaweza kuwa painia musaidizi mara kwa mara? Iwe unaweza kuwa painia ao hapana, tuko hakika kwamba Yehova atakubariki kwa sababu ya kujitoa ili kufanya mengi zaidi katika kutangaza Ufalme.—Mal. 3:10.
6. Sababu gani Mwezi wa 10, 2014 utakuwa wa pekee sana?
6 Katika Mwezi wa 10 2014 Ufalme utaeneza miaka 100 tangu ulianza kutawala. Inafaa kabisa kwa sababu toleo la watu wote la Munara wa Mulinzi la mwezi huo linazungumuzia sana Ufalme. Tujikaze sana ili kuwatolea watu wengi zaidi gazeti hilo. Tunapoendelea kungojea wakati unaokuja, acheni kila mumoja wetu aendelee ‘kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu’ kwa wote walio tayari kusikiliza.—Matendo 8:12.