TUNGO LA MWEZI: “LIHUBIRI NENO, FANYA HIVYO KWA BIDII [KWA HARAKA].”—2 TIM. 4:2.
Tuelezee Watu Mambo Ambayo Tunaamini Kuhusu Mwaka wa 1914
Biblia inatutia moyo tuwe ‘tayari kutetea’ imani yetu, lakini tufanye hivyo “kwa tabia-pole na heshima kubwa.” (1 Pet. 3:15) Ni kweli kwamba inaweza kuwa vigumu kwetu kufasiria mafundisho mazito ya Biblia, kama vile, namna gani tunajua kwamba Ufalme ulianza kutawala katika mwaka wa 1914. Ili kutusaidia tuelezee watu imani yetu juu ya mwaka huo, habari yenye kichwa Mazungumuzo ya Biblia Pamoja na Jirani—Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? imetayarishwa. Habari hiyo ina sehemu mbili ambazo zinapatikana katika magazeti Munara wa Mulinzi za kutolea watu katika Mwezi wa 10 na wa 11. Unaposoma habari hizo, fikiria maulizo yanayofuata kuhusu ufundi ambao muhubiri anayeitwa Richard anatumia katika mazungumuzo hayo.
Namna gani Ndugu Richard . . .
anamushukuru mara kwa mara musikilizaji ili kufanya mazungumuzo yaendelee vizuri?—Mdo. 17:22.
anaonyesha unyenyekevu wakati anafasiria mambo ambayo anaamini?—Mdo. 14:15.
Sababu gani Ndugu Richard anafanya vizuri kwa . . .
kurudilia kwa kifupi mambo aliyosema, mbele ya kuzungumuzia mambo mengine?
kutua mara kwa mara ili kumuuliza musikilizaji ikiwa anaelewa mambo ambayo amekwisha kumufasiria?
kutoeleza mambo mengi sana mara moja tu?—Yoh. 16:12.
Tunamushukuru sana Yehova, ambaye ni ‘Mufundishaji Wetu Mukubwa,’ kwa sababu anatufundisha namna ya kueleza Mafundisho ya Biblia kwa watu wote walio na njaa!—Isa. 30:20.