Tolea Wengine ‘Mambo Mazuri’: Uwe Mukaribishaji-Wageni (Mt. 12:35a)
Bila shaka sisi wote tunapenda kutolea wengine “mambo mema [mazuri]” kwa kufuata “mwendo wa ukaribishaji-wageni.” (Rom. 12:13) Wazee wameombwa kuwa mufano muzuri katika jambo hilo. Wakati kuna musemaji mugeni katika kutaniko, wazee wanafanya mupango ili akaribishwe muzuri, na kuhakikisha kwamba feza ambazo alitumia ili kusafiri zinalipwa. Hata hivyo, mutu anaweza kusita kuonyesha ukarimu kwa sababu hana uwezo, ao anaweza kuogopa kuwaalika wengine kwake. Ikiwa tunakumbuka maneno ambayo Yesu alimuambia Martha, tunaweza kumaliza tatizo hilo. (Luka 10:39-42) Yesu alionyesha kwamba ‘fungu jema’ la kuwakaribisha wengine ni kupitisha wakati nao na kutiana moyo, haiko chakula kilichotayarishwa vizuri ao nyumba iliyopambwa muzuri. Ikiwa sisi wote tunatumikisha shauri hili, tunaweza kuwatolea ndugu zetu ‘mambo mazuri’ kupatana na Neno la Mungu.—3 Yoh. 5-8.