Programu ya Juma la Tarehe 29 Mwezi wa 12
JUMA LA TAREHE 29 MWEZI WA 12
Wimbo 37 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 18 fu. 1-8 (Dak. 30)
Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 12-15 (Dak. 10)
Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi (Dak. 20)
Mukutano wa Utumishi:
Tungo la Mwezi: Tutoe “mambo mema [mazuri]” kutoka katika hazina nzuri ambayo tumepewa.—Mt. 12:35a.
Wimbo 89
Dak. 20: Fundisha Wanafunzi wa Biblia na Watoto Wako ‘Mambo Mazuri’ Hatua kwa Hatua. (Mt. 12:35a) Mazungumuzo. Tumia maandiko ambayo yanafuata ili kuonyesha yale ambayo tunapaswa kutazamia kwa wanafunzi wa Biblia na watoto wetu: 1 Wakorintho 13:11; 1 Petro 2:2, 3. Fasiria maana ya ‘kuonja maziwa ya lile Neno,’ na namna tunaweza kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia na watoto wetu kufanya hivyo. Fasiria kanuni iliyo kwenye Marko 4:28. (Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 12, 2014, uku. 12, fu. 6-8.) Umuombe muhubiri mwenye uzoefu ao muzazi aeleze namna alimusaidia mwanafunzi ao mutoto afanye maendeleo ya kiroho.—Efe. 4:13-15; soma Kisanduku cha Maulizo kilicho katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 5, 2014.
Dak. 10: “Tolea Wengine ‘Mambo Mazuri’: Uwe Mukaribishaji-Wageni (Mt. 12:35a).” Mazungumuzo. Mumepata faida gani ao mumejionea mambo gani mazuri kwa sababu ya kuwakaribisha wageni kwenu? Waombe wasikilizaji waeleze namna tunaweza kutolea wengine ‘mambo mazuri’ kwa kuwakaribisha kwetu, zaidi sana wale walio katika utumishi wa wakati wote. Zungumuzia mupango wa kumukaribisha musemaji mugeni ili kula pamoja naye nyumbani.
Wimbo 124 na Sala