Tuwasaidie Vipofu Wajifunze Juu ya Yehova
1. Yesu alifanya nini ili kuonyesha kama anasikilia vipofu huruma?
1 Wakati Yesu alikuwa anatoka Yeriko siku fulani mbele ya kifo chake, vipofu wawili walimuomba kwa sauti kubwa: ‘Bwana, utuhurumie!’ Hata kama Yesu alihangaishwa sana na mateso yenye yalikuwa yanamungojea, alisimama, akawaita wanaume hao na akafungua macho yao. (Mat. 20:29-34) Yesu aliwasikilia vipofu hao huruma. Namna gani tunaweza kumuiga?
2. Namna gani tunaweza kuhubiri kipofu mwenye tunakutana mahali pa watu wengi?
2 Ukuwe Tayari Kuwasaidia: Wakati unakutana kipofu, hata mahali pa watu wengi, ujitambulishe kwake na umuambie kama unataka kumusaidia. Kwa sababu watu wanawaonea vipofu, inawezekana asikuone kuwa rafiki wakati unazungumuza naye kwa mara ya kwanza. Lakini ukionesha kama unamuhangaikia kabisa, anaweza kukuona kuwa rafiki. Tena, ujue kama kuna aina nyingi za upofu, na kujua jambo hilo kutakusaidia utambue musaada wa kutoa. Kisha kumusaidia, unaweza sasa kumuambia kama unafanya kazi ya kufundisha watu Biblia. Umuambie kama unapenda kumusomea andiko fulani, kwa mufano Zaburi 146:8 ao Isaya 35:5, 6. Kama iko na uwezo wa kusoma maandishi ya vipofu, umuulize kama angependa kupata kichapo cha maandishi ya vipofu chenye kitamusaidia kujifunza mengi zaidi juu ya Biblia. Unaweza pia kumusaidia kupata habari ya kusikiliza tu kutoka jw.org. Kama ordinatere yake iko na programu ya kusoma maandishi kwa sauti, inaweza kuwa muzuri kuchukua habari fulani kwenye jw.org kati ya vichapo vyenye vinaweza kuchukuliwa kwa forma ya RTF.—Ona kisanduku “Wakati Unasaidia Kipofu . . .
3. Namna gani tunaweza kuwatafuta vipofu katika eneo letu?
3 Tuwatafute Vipofu: Haiko vyepesi kuzungumuza na vipofu wakati tunahubiri nyumba kwa nyumba kwa sababu vipofu wengi wanakuwa na wasiwasi wakati watu wenye hawajue wanawatembelea. Kwa hiyo, inaomba kuwa na bidii ili kuwatafuta na kuwahubiria. (Mat. 10:11) Unajua mufanya kazi ao mwanafunzi mwenzako mwenye iko kipofu? Kamata mupango wa kuzungumuza naye. Kama katika eneo lenu kuna masomo kwa ajili ya vipofu, tolea masomo hiyo vichapo fulani katika maandishi ya vipofu. Unajua mutu fulani mwenye anaishi na kipofu katika jamaa yake? Katika eneo lenu kuna mashirika yenye kuwasaidia vipofu na watu wenye kuchunga vipofu? Kama jibu ni ndiyo, umufasirie mutu huyo, ao mutu mwenye kupokea wageni katika mashirika hayo, ao musimamizi wa mashirika hayo kwamba Mashahidi wa Yehova wanapenda kuwasaidia vipofu, na uwatolee maandishi ao habari ya kusikiliza kwa ajili ya vipofu. Umuonyeshe kipofu ahadi ya Biblia ya kwamba karibuni Mungu atafungua macho ya vipofu ili wapate kuona milele. Ukipenda unaweza pia kumusikilizisha video yenye kichwa “Sans Elle, Je Serais Perdu.” Video hiyo inapatika kwenye jw.org na inaeleza maisha ya mwanaume kipofu mwenye amefaidika sana kwa sababu amepata Biblia katika maandishi ya vipofu. Wakati tunawatembelea vipofu, tuwaambie mara moja sababu gani tunawatembelea; tukifanya hivyo vipofu wanaweza kutukaribisha.
4. Habari ya dada Janet inatufundisha nini?
4 Dada mumoja kipofu anayeitwa Janet alitembelea nyumba ya vipofu. Alianzisha mazungumuzo na mwanamuke kijana mumoja. Janet alimuambia hivi: “Yesu alifungua macho ya vipofu ili kuonyesha mambo yenye karibuni atafanyia vipofu wote.” Wakasoma pamoja andiko la Ufunuo 21:3, 4, na Janet akafasiria namna gani ahadi yenye kuwa katika andiko hilo itatimizwa kupitia Ufalme wa Mungu. Mwanamuke huyo akanyamaza na kisha akasema: “Ni mara ya kwanza kusikia maneno kama haya kutoka kwa kipofu mwenzangu. Watu wengi wenye hawako vipofu wanawaza kama tuko vipofu kwa sababu siye ao wazazi wetu walimukosea Mungu.” Janet alimuandikia mwanamuke huyo kupitia Internete na katika barua hiyo akamuonyesha namna ya kupata kitabu Biblia Inafundisha kwenye Internete, na sasa wanajifunza Biblia mara mbili kila juma.
5. Hata kama hatuna uwezo wa kufungua macho ya vipofu kama vile Yesu alifanya, namna gani tunaweza kuwasaidia?
5 Yesu alifungua macho ya vipofu; siye hatuna uwezo huo, lakini tunaweza kufungua macho ya vipofu wa mufano, ni kusema, watu wenye mungu wa dunia hii amepofusha akili yao; kati yao kuna pia vipofu wa kweli. Tunaweza kuwasaidia waone ukweli wa Neno la Mungu. (2 Kor. 4:4) Yesu alifungua macho ya wanaume vipofu wawili karibu na Yeriko kwa sababu aliwasikilia huruma. (Mat. 20:34) Kama tunafuata mufano wa Yesu, tunaweza pia kufurahia pendeleo la kuwasaidia wamoja wao kumujua Yehova, Mungu mwenye karibuni atafungua macho ya vipofu ili wapate kuona milele.