Vyombo Mbalimbali vya Kutusaidia Kufundisha
1. Ni katika njia gani Wakristo wanafanana na mafundi?
1 Mafundi wanatumia vyombo mbalimbali ili kutimiza kazi fulani. Vyombo fulani vinatumiwa tu ili kutimiza kazi fulani ya pekee na vingine vinatumiwa sana. Mara nyingi, mafundi wenye uzoefu wanapanga vyombo vyenye vinatumiwa sana katika kisanduku fulani, na wanajua kuvitumia muzuri zaidi kuliko vyombo vingine. Biblia inatia moyo kila Mukristo afanye kazi ya kuhubiri na akuwe ‘mufanya kazi asiye na lolote la kuonea aibu.’ (2 Tim. 2:15) Kati ya vyombo vyenye kutusaidia kufundisha, ni chombo gani cha maana zaidi tunatumia? Ni Neno la Mungu; tunatumia sana Neno la Mungu ili ‘kufanya wanafunzi.’ (Mt. 28:19, 20) Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza kuwa wenye ufundi ili ‘kutumia sawasawa neno la kweli.’ Lakini, kati ya vyombo vyetu mbalimbali, kuna vyombo vingine vyenye tunatumia sana ili kufundisha watu kweli. Kila Mukristo anapaswa kujua kutumia vyombo hivyo kwa ufundi.—Met. 22:29.
2. Ni vyombo gani tunatumia sana ili kufundisha?
2 Vyombo Vyenye Tunatumia Sana ili Kufundisha: Kama vile tumeona, Biblia ni chombo cha maana zaidi chenye tunatumia. Lakini, ni vyombo gani vingine tunapaswa kutumia? Chombo kingine chenye tunatumia sana ili kufundisha kweli za Biblia ni kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kisha kumaliza kujifunza na mutu kupitia kitabu hicho, tunatumia kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu” ili kumufundisha namna ya kutumikisha kanuni za Biblia katika maisha yake ya kila siku. Kwa hiyo, tunapaswa kutumia vitabu hivyo viwili kwa ufundi. Tunatumia pia broshua fulani ili kufundisha watu Biblia. Kwa mufano, broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! ni chombo chenye tunatumia sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tunaweza pia kutumia broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, ili kufundisha watu wenye hawana uwezo wa kusoma muzuri, wale wenye tuko na vichapo kidogo ao hatuna vichapo katika luga yao. Chombo chenye tunatumia sana ili kumuongoza mwanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo ni broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Video kama vile Sababu gani Ujifunze Biblia?, Ni Mambo Gani Inafanyikaka Kwenye Jumba la Ufalme?, na Je, Mungu Ana Jina?, zinaweza pia kutusaidia katika kazi ya kufanya wanafunzi. Kwa hiyo, tunapaswa kujua namna ya kutumia video hizo muzuri.
3. Katika siku zenye kuwa mbele, Huduma Yetu ya Ufalme itatusaidia kufanya nini?
3 Katika siku zenye kuwa mbele, Huduma Yetu ya Ufalme itatuonyesha namna ya kutumikisha vichapo fulani kati ya vile tunatumia sana ili kufundisha watu Biblia. Ikiwa tunajikaza kutumia vyombo hivyo kwa ufundi, tutaonyesha kwamba tunafuata shauri hili lenye kuongozwa na roho ya Mungu: ‘Ujiangalie daima wewe mwenyewe na kufundisha kwako. Kaa katika mambo haya, kwa maana kwa kufanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaokusikiliza pia.’—1 Tim. 4:16.