“Maneno Haya . . . Lazima Yakuwe Katika Moyo Wako”
Wazazi wako kama wachungaji. Wanapaswa kuchunga watoto wao muzuri kwa sababu wanaweza kupotea kwa urahisi na kujitia katika hatari. (Met. 27:23) Namna gani wazazi wanaweza kutimiza daraka lao la kuchunga watoto? Kila siku, wanapaswa kuwa na wakati wa kuzungumuza na watoto wao ili kujua mambo yenye kuwa katika akili zao na katika mioyo yao. (Met. 20:5) Wazazi wanapaswa pia kutumia vifaa vyenye haviwezi kuungua ili kufanya imani ya watoto wao ikuwe yenye nguvu. (1 Kor. 3:10-15) Video ‘Maneno Haya . . . Lazima Yakuwe Katika Moyo Wako,’ inaonyesha kwamba ni jambo la maana sana kufanya ibada ya familia kwa ukawaida. Mufuate video hiyo katika familia yenu na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.
(1) Ni nini ilifanya familia ya Toma ikose kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza? (2) Sababu gani mwanzoni Ndugu Toma alishindwa kukusanya familia kwa ajili ya ibada? (3) Ni mwongozo gani wa Biblia unaweza kusaidia wazazi kulea watoto wao muzuri? (Kum. 6:6, 7) (4) Ni nini inaweza kusaidia familia ikuwe na mazungumuzo mazuri? (5) Watoto wanapenda wazazi wao wafanye nini? (6) Namna gani ndugu Martin na bibi yake walisaidia familia ya Toma? (Met. 27:17) (7) Baba wa familia anapaswa kufanya nini kwanza ili ibada ya familia ikuwe na matokeo mazuri? (8) Namna gani Ndugu Toma alianza kutengeneza mambo katika familia yake? (9) Sababu gani ni jambo la maana sana kuheshimia programu ya ibada ya familia? (Efe. 6:4) (10) Taja mambo fulani yenye tunaweza kufanya katika ibada ya familia. (11) Wakati Ndugu Toma alimusaidia Marc aone kwamba ni jambo la lazima kufanya mambo mazuri, namna gani alionyesha utulivu lakini bila kubembeleza? (Yer. 17:9) (12) Namna gani Ndugu Toma na bibi yake walifikiri pamoja na Rebeka ili kumusaidia achukue uamuzi muzuri kuhusu urafiki wake pamoja na Justin? (Mk. 12:30; 2 Tim. 2:22) (13) Namna gani Ndugu Toma na bibi yake walionyesha imani wakati waliamua kufanya mabadiliko katika maisha yao? (Mt. 6:33) (14) Namna gani video hii inaonyesha kwamba ni lazima baba wa familia watimize mahitaji ya kiroho ya familia zao? (1 Tim. 5:8) (15) Kwa kuwa wewe ni baba wa familia, umeamua kufanya nini?
KWA BABA WA FAMILIA: Muchezo huu wenye kutegemea Biblia, ulichezwa kwenye mikusanyiko ya eneo (ao ya wilaya wakati huo) yenye ilifanyika katika mwaka wa 2011. Wakati mulifuata muchezo huo, mulitambua mambo yenye munapaswa kufanya ili ibada yenu ya familia ikuwe muzuri zaidi? Ibada yenu ya familia iko namna gani leo? Ikiwa munaona kwamba kungali mabadiliko mengine ya kufanya, musali ili Yehova awasaidie kufanya mabadiliko hayo.Hilo litaletea familia yenu faida ya milele.—Efe. 5:15-17.