Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/12
“Tunatembelea majirani wetu ili kuzungumuza nao juu ya mawazo mabaya yenye watu wengi wako nayo juu ya Biblia. Watu wengi wanaheshimia Biblia, lakini wanawaza kwamba haieleweke. Weye, unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Tafazali, acha nikuonyeshe sababu gani ni lazima tujikaze kuelewa Biblia. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linaonyesha sababu gani tunajua kwamba Biblia iliandikwa ili tuielewe na linaonyesha pia mambo fulani ya kufanya ili tuielewe.”
Amuka! Mwezi wa 12
“Tunawatembelea kwa muda mufupi ili kuzungumuza na nyiye juu ya habari ya maana kuhusu familia. Kila mutu anataka amani na upatano katika nyumba yake. Unawaza inaomba kufanya nini? Kujaribu kuepuka kila hali yenye inaweza kuvuruga amani, ao kujifunza muzuri zaidi kufanya amani katika familia? [Acha mutu ajibu.] Tuone kama mezali moja ya Biblia inasema nini. [Soma Methali 26:20.] Gazeti hili linazungumuzia mashauri fulani ya Biblia yenye kusaidia watu wakuwe na amani katika familia zao.”