UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZRA 6-10
Yehova Anapenda Watu Wenye Kuwa Tayari Kumutumikia
Ezra alifanya matayarisho ya kurudia Yerusalemu
7:6, 22; 8:26, 27
Mufalme Artashasta anamuruhusu Ezra arudie Yerusalemu ili kuendelesha ibada ya Yehova
Mufalme anamupa mambo yote yenye aliomba kwa ajili ya nyumba ya Yehova—zahabu, feza, ngano, divai, mafuta, na chumvi, vyote vilikuwa zaidi ya dolare 100 000 000 za Amerika za siku za leo
Ezra alikuwa hakika kwamba Yehova atalinda watumishi Wake
7:13; 8:21-23
Kurudia katika Yerusalemu haikukuwa mwepesi
Pengine njia hiyo ilikuwa na urefu wa kilometre 1 600 hivi katika eneo lenye hatari nyingi
Safari ilikuwa ya miezi 4 hivi
Wale wenye walirudia walihitaji kuwa na imani yenye nguvu, bidii kwa ajili ya ibada ya kweli, na kutokuwa na woga
EZRA ALISAFIRI NA . . .
Zahabu na feza yenye kuwa na uzito wa zaidi ya talanta 750 Uzito wa tembo dume tatu hivi wa Afrika wenye kukomaa
MAGUMU YENYE WALE WENYE WALIRUDIA WALIPAMBANA NAYO . . .
Vikundi vya wanyanganyi, jangwa, vidudu na nyama wa pori