Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 9 uku. 7
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Saidia Wanafunzi Wako wa Biblia Wahuzurie Mikutano
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 9 uku. 7

MAISHA YA MUKRISTO

TUKOMALISHE UFUNDI WETU WA KUHUBIRI —Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano

Ndugu anatolea mwanaume mualiko kwa ajili ya mikutano

SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO: Kwenye mikutano yetu tunapata nafasi ya ‘kumuimbia Yehova’ na kumusifu mara kwa mara. (Zab 149:1) Kwenye mikutano tunafundishwa kufanya mapenzi ya Mungu. (Zab 143:10) Mara nyingi watu wenye kupendezwa na wenye kujifunza Biblia wanafanya maendeleo wakati wanaanza kufika kwenye mikutano.

TOLEO LA MWEZI WA 10: MUALIKO KWA AJILI YA MIKUTANO YA KUTANIKO

Watu fulani wenye walikuja kwenye mikutano yetu kwa mara ya kwanza, wamefikia kusema hivi: “Mungu yupo katikati yenu.” (1Kor 14:25) Katika mwezi wa 10 tutajikaza sana kualika watu kwenye mikutano yetu ya mwisho wa juma. Tutawatolea mualiko kwa ajili ya mikutano, na kama musikilizaji anakubali tunaweza kumuonyesha video Kwa Kawaida, Ni Mambo Gani Inafanyika Kwenye Jumba la Ufalme? Juma lenye kufuata tutaona na kuzungumuzia video yenye kuonyesha namna ya kufanya hivyo.

NAMNA YA KUFANYA:

  • Ualike watu bila kukawia. Haiko lazima ungojee mupaka wakati mutaanza funzo la Biblia.—Ufu 22:17

  • Mashahidi wa Yehova wanaingia katika Jumba la Ufalme

    Elezea mutu mwenye kupendezwa namna mikutano inapitika na habari yenye itazungumuziwa kwenye mikutano yenye kufuata. Mambo haya yanaweza kukusaidia kufanya hivyo: mualiko kwa ajili ya mikutano, video Kwa Kawaida, Ni Mambo Gani Inafanyika Kwenye Jumba la Ufalme?, na sura ya 5 na ya 7 ya broshua Mapenzi ya Yehova

  • Ndugu anasoma Biblia pamoja na mwanaume mwenye kupendezwa

    Unaweza kusaidia mutu mwenye kupendezwa kufika kwenye mikutano ao kuchagua nguo yenye kufaa. Ukae pembeni yake kwenye mikutano, na mutumie pamoja vichapo vyako. Umutambulishe kwa wengine

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine