MAISHA YA MUKRISTO
TUKOMALISHE UFUNDI WETU WA KUHUBIRI —Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano
SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO: Kwenye mikutano yetu tunapata nafasi ya ‘kumuimbia Yehova’ na kumusifu mara kwa mara. (Zab 149:1) Kwenye mikutano tunafundishwa kufanya mapenzi ya Mungu. (Zab 143:10) Mara nyingi watu wenye kupendezwa na wenye kujifunza Biblia wanafanya maendeleo wakati wanaanza kufika kwenye mikutano.
NAMNA YA KUFANYA:
Ualike watu bila kukawia. Haiko lazima ungojee mupaka wakati mutaanza funzo la Biblia.—Ufu 22:17
Elezea mutu mwenye kupendezwa namna mikutano inapitika na habari yenye itazungumuziwa kwenye mikutano yenye kufuata. Mambo haya yanaweza kukusaidia kufanya hivyo: mualiko kwa ajili ya mikutano, video Kwa Kawaida, Ni Mambo Gani Inafanyika Kwenye Jumba la Ufalme?, na sura ya 5 na ya 7 ya broshua Mapenzi ya Yehova
Unaweza kusaidia mutu mwenye kupendezwa kufika kwenye mikutano ao kuchagua nguo yenye kufaa. Ukae pembeni yake kwenye mikutano, na mutumie pamoja vichapo vyako. Umutambulishe kwa wengine