Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 3 uku. 7
  • Neno la Mungu Limebadilishwa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Neno la Mungu Limebadilishwa?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NI NINI INATUHAKIKISHIA KAMA MAANDIKO MATAKATIFU YENYE TUKO NAYO LEO IKO NA UJUMBE WA KWANZA-KWANZA WA MUNGU?
  • Biblia Imebadilishwa ao Kugeuzwa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • A3 Namna Biblia Ilitufikia
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Ukuwe Hakika Kama ‘Neno la Mungu Ni Kweli’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Biblia Iliokoka Hata Kama Watu Walijaribu Kubadilisha Ujumbe Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 3 uku. 7
Sehemu ya kitabu cha Isaya ya Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi yenye kuwa juu ya tafsiri ya sasa ya Kiarabu ya kitabu cha Isaya

Sehemu ya kitabu cha Isaya ya Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi yenye kuwa juu ya tafsiri ya sasa ya Kiarabu ya kitabu cha Isaya. Ujumbe wa Neno la Mungu haujabadilishwa

Neno la Mungu Limebadilishwa?

Watu fulani wanajiuliza kama Neno la Mungu halijabadilishwa. Nabii Isaya alisema kama neno la Mungu “linadumu milele.” (Isaya 40:8) Ni nini inatuhakikishia kama ahadi za Mungu hazijabadilishwa?

Mungu iko na uwezo wa kulinda Neno lake na kuzuia watu wasilibadilishe. Zamani, wenye walikuwa wanafanya kopi za maandishi matakatifu, walikuwa wanahesabia kwa uangalifu kila herufi juu ya kuhakikisha kama hakuna kitu chenye kiliongezwa, kubadilishwa, ao kuachwa. Lakini juu wanadamu hawakamilike, wamoja kati ya wenye walikuwa wanafanya kopi za maandishi matakatifu waliingiza makosa kidogo.

NI NINI INATUHAKIKISHIA KAMA MAANDIKO MATAKATIFU YENYE TUKO NAYO LEO IKO NA UJUMBE WA KWANZA-KWANZA WA MUNGU?

Kuko maelfu ya kopi za maandishi ya zamani ya Maandiko Matakatifu. Ni mwepesi kuvumbua kwenye kuko kosa kwa kulinganisha kopi mbalimbali.​—Ikiwa unapenda kujua mingi zaidi, ona habari “Biblia Imebadilishwa ao Kugeuzwa?” ku jw.org.

Kwa mufano, tufikirie maandishi ya zamani yenye inaitwa Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi, vyenye Wabedui walivumbua katika mapango (caves) fulani karibu na Bahari ya Chumvi mu mwaka wa 1947. Ile maandishi iko na sehemu za Maandiko Matakatifu ya tangu miaka zaidi ya elfu mbili. Wasomi walilinganisha ile maandishi ya zamani na Maandiko Matakatifu yenye tuko nayo leo. Walivumbua nini?

Walivumbua kama habari zenye ziko mu Neno la Mungu lenye tuko nalo leo njo zilezile zenye zilikuwaka mu maandishi ya kwanza-kwanza.a Kuchunguza maandishi ya zamani kunahakikisha kama mambo yenye tunasoma mu Maandiko Matakatifu njo ujumbe wenye Mungu alitolea wanadamu ku mwanzo. Tunaweza kuwa hakika kama Mungu amelinda kwa uangalifu Maandishi Matakatifu ili ujumbe wake usibadilishwe.

Kwa hiyo, tunaweza kusoma Neno la Mungu na tuko hakika kabisa kama ujumbe wake haujabadilishwa. Kisha kujua ile, tuchunguze sasa mambo yenye manabii wanaweza kutufundisha kumuhusu Mungu.

a The Complete Dead Sea Scrolls in English, cha Geza Vermes, ukurasa wa 16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine