UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ISAYA 63-66
Mbingu Mupya na Dunia Mupya Vitaleta Furaha Kubwa Sana
Ahadi ya Mungu yenye kuwa katika Isaya 65 kuhusu kurudisha dunia katika hali yake ya kwanza itatimia kabisa; ndiyo sababu Yehova anaizungumuzia kama vile imekwisha kutimia.
Yehova anaumba mbingu mupya na dunia mupya, na humo, mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini
Mbingu mupya ni nini?
Serikali ao guvernema mupya yenye italeta haki katika dunia
Ilianza kutawala katika mwaka wa 1914, wakati Kristo alifanywa kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu
Dunia mupya ni nini?
Watu wa mataifa yote, luga zote, na rangi zote za ngozi, wenye wanakubali kutawaliwa na serikali mupya ya mbinguni
Ni katika njia gani mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini?
Mateso ya kimwili, kiakili, na ya moyoni yenye kutuumiza wakati tunayakumbuka hayatakuwa tena
Wanadamu waaminifu watafurahia kabisa maisha, na kila siku watakumbuka mambo yenye kupendeza