Ndugu anatoa trakte Watu Waliokufa Wanaweza Kweli Kuishi Tena? ya Kituvalu
Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
AMUKA!
Ulizo: Sababu gani ni jambo la maana kujitayarisha kwa ajili ya misiba?
Andiko: Met 27:12
Namna ya Kutoa: Gazeti hili linaonyesha mambo tunaweza kufanya mbele ya musiba, wakati wa musiba, na kisha musiba.
FUNDISHA KWELI
Ulizo: Tunaonyesha namna gani kama tunamupenda Mungu?
Andiko: 1Yoh 5:3
Kweli: Tunaonyesha kama tunamupenda Mungu kwa kutii amri zake.
WATU WALIOKUFA WANAWEZA KWELI KUISHI TENA? (T-35)
Ulizo: Katika dunia yote, kila mwaka watu wengi wanafanya sikukuu za kukumbuka watu wenye wamekufa. Tunaweza kuwa na tumaini la kuona tena wapendwa wetu wenye wamekufa?
Andiko: Mdo 24:15
Namna ya Kutoa: Trakte hii inazungumuzia faida yenye tumaini la ufufuo linaweza kukuletea. [Kama inawezekana, umuonyeshe mutu video Kuko Tumaini kwa Ajili ya Watu Wenye Wamekufa?]
ANDIKA NAMNA UNAWEZA PIA KUANZISHA MAZUNGUMUZO
Fuata mufano wenye kuwa hapo juu ili kuandika namna yako ya kuanzisha mazungumuzo.