MAISHA YA MUKRISTO
Mambo Yenye Tunajifunza Katika Kitabu cha Yona
Yehova ameandikisha katika Neno lake, habari za wanaume na wanamuke wenye imani ili kutufundisha mambo ya maana. (Rom 15:4) Kitabu cha Yona kimekufundisha nini? Muangalie video Ibada ya Familia: Yona—Tuige Rehema ya Yehova, kisha mujibie maulizo haya:
Wahubiri watatu wenye tumeona katika video, walipata magumu gani?
Kama tumekaripiwa ao tumepoteza mapendeleo fulani, namna gani habari ya Yona inaweza kutusaidia? (1Sam 16:7; Yona 3:1, 2)
Namna gani habari ya Yona inaweza kutusaidia tukuwe na mawazo ya muzuri juu ya watu wa eneo letu? (Yona 4:11; Mt 5:7)
Kama tuko na ugonjwa fulani wenye unakataa kupona, namna gani habari ya Yona inaweza kututia moyo? (Yona 2:1, 2, 7, 9)
Video hii imekusaidia namna gani uone faida ya kusoma Biblia na kuwaza sana juu ya mambo yenye unasoma?