Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 3 uku. 7
  • “Endelea Kukesha”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Endelea Kukesha”
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Utaendelea Kukesha’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mufano wa Mabikira Kumi—Somo Kuhusu Kukesha
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Ukuwe Muangalifu, Usikilize Onyo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Ule Mwenye Kuvunja Sheria Anafunuliwa
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 3 uku. 7
Mabikira kumi wa mufano wa Yesu

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 25

“Endelea Kukesha”

25:1-12

Hata kama mufano wa Yesu wa mabikira kumi ulihusu kwanza wanafunzi wake watiwa-mafuta, somo lenye kupatikana katika mufano huo linahusu Wakristo wote. (w15 15/3 uku. 12-16) ‘Kwa hiyo, muendelee kukesha kwa sababu hamuijue ile siku wala saa.’ (Mt 25:13) Unaweza kufasiria mufano huo wa Yesu?

  • Bwana-arusi (mustari wa 1)​—Yesu

  • Mabikira wenye busara, wenye kuwa tayari (mustari wa 2)​—Wakristo watiwa-mafuta wenye wako tayari kutimiza mugao wao kwa uaminifu na wenye wanaangaza kama mianga mupaka mwisho (Flp 2:15)

  • Sauti kubwa: “Bwana-arusi anafika!” (mustari wa 6)​—Alama ya kuwapo kwa Yesu

  • Mabikira wapumbavu (mustari wa 8)​—Wakristo watiwa-mafuta wenye wanatoka ili kukutana na Bwana-arusi lakini hawaendelee kukesha na wanakosa kuwa washikamanifu

  • Mabikira wenye busara wanakataa kupatia wengine mafuta yao (mustari wa 9)​—Kisha kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho, watiwa-mafuta waaminifu hawatakuwa tena na wakati wa kusaidia watiwa-mafuta wenye walikosa kuwa waaminifu

  • “Bwana-arusi akafika” (mustari wa 10)​—Yesu anakuja kuleta hukumu karibu na mwisho wa ziki kubwa

  • Mabikira wenye busara wanaingia pamoja na bwana-arusi kwenye karamu ya ndoa, na mulango unafungwa (mustari wa 10)​—Yesu anakusanya watiwa-mafuta wake waaminifu mbinguni, lakini watiwa-mafuta wenye walikosa kuwa waaminifu wanapoteza zawadi yao ya kuenda mbinguni

Yesu hakupenda kusema kama Wakristo wengi watiwa-mafuta watakosa kuwa waaminifu na kama wengine watachukua nafasi yao. Lakini, mufano huo wa Yesu unatoa onyo kwamba kila Mukristo mutiwa-mafuta anapaswa kuchagua kama atakuwa tayari na ataendelea kuwa macho ao kama atakuwa mupumbavu na kukosa uaminifu. Yesu alishauri hivi: ‘Mukuwe tayari.’ (Mt 24:44) Ikuwe tuko na tumaini la kuishi mbinguni ao duniani, Yesu anatuomba sisi wote tutayarishe moyo wetu ili kufanya kazi kwa uaminifu, na anatuomba sisi wote tuendelee kukesha.

Ninaonyesha namna gani kama ninaendelea kukesha?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine