Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 6 uku. 7
  • Epuka Hatari ya Kutumia Site za Enternete za Kupashana Habari

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Epuka Hatari ya Kutumia Site za Enternete za Kupashana Habari
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unajua Marafiki Wako wa ku Enternete?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Mukubwa Fulani wa Mambo ya Afya Anaonya Kuhusu Hatari ya Site za Kupashana Habari kwa Vijana​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Usijifikirie Mwenyewe Sana Kuliko Vile Inaomba Kufikiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Teknolojia Iko na Matokeo Gani Juu ya Urafiki Wako na Wengine?
    Amuka!—2021
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 6 uku. 7

MAISHA YA MUKRISTO

Epuka Hatari ya Kutumia Site za Enternete za Kupashana Habari

Yesu anakataa kugeuza majiwe kuwa mikate

SABABU GANI NI LAZIMA: Site za enternete za kupashana habari zinaweza kutusaidia ao kutuumiza. Wakristo fulani wameamua kukataa kabisa kutumia site hizo. Wakristo wengine wanazitumia ili kupashana habari na watu wa familia zao na marafiki. Lakini, Ibilisi anapenda tutumie site za kupashana habari bila hekima. Hilo linaweza kutuharibishia sifa na kutuharibishia urafiki wetu pamoja na Yehova. Kama Yesu, tunaweza kutumia kanuni zenye kupatikana katika Neno la Mungu ili kutambua hatari na kuziepuka.​—Lu 4:4, 8, 12.

MITEGO YA KUEPUKA:

  • Kutumia site za enternete za kupashana habari kupita kiasi. Kutumia site za enternete za kupashana habari na vyombo vya kutangaza habari kwa saa murefu kunaweza kuchukua wakati wenye tunapaswa kutumia kwa ajili ya mambo ya kiroho

    Kanuni za Biblia: Efe 5:15, 16; Flp 1:10

  • Kuangalia mambo ya mubaya. Kuangalia mambo ya mubaya kunaweza kuchochea mutu akuwe mutumwa wa ponografia ao afanye uasherati. Kusoma vitabu vya waasi-imani ao habari zao kwenye Enternete kunaweza kuharibu imani ya mutu

    Kanuni za Biblia: Mt 5:28; Flp 4:8

  • Kutia picha ao maelezo ya mubaya kwenye site hizo. Kwa sababu moyo ni mudanganyifu, mutu anaweza kushawishiwa kutia maelezo ya mubaya ao picha za mubaya kwenye site za kupashana habari. Hilo linaweza kuharibishia mutu sifa ao kufanya wengine wakwazike

    Kanuni za Biblia: Rom 14:13; Efe 4:29

MUANGALIE VIDEO TUMIA KWA HEKIMA SITE ZA ENTERNETE ZA KUPASHANA HABARI, KISHA MUZUNGUMUZIE NAMNA YA KUEPUKA HALI KAMA HIZI:

Mwizi mwenye anatumia pia site za enternete za kupashana habari anajua kama mwenye nyumba ameenda safari
Mukubwa wa kazi anaona picha zenye hazifae za mutu mwenye anatafuta kazi
Hatari ya kusikiliza maneno machafu kwenye site za enternete za kupashana habari
Kijana huyu alitumia vyombo vya kupashana habari mupaka usiku sana; sasa anashindwa kulamuka asubui
    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine