MAISHA YA MUKRISTO
Unajua Marafiki Wako wa ku Enternete?
Rafiki ni “mutu mwenye anaambatana na mwingine juu anamupenda ao anamusamini.” Kwa mufano, Yonatani na Daudi walianzisha urafiki wa kufa na kupona kisha tu Daudi kumuua Goliati. (1Sa 18:1) Kila mumoja wao alikuwa na sifa zenye zilivutia mwingine. Ile inaonyesha kama urafiki wa kweli ni kujuana muzuri. Kujua mutu muzuri inaombaka wakati na nguvu. Lakini, ku site za Enternete za kupashana habari ni mwepesi mukuwe marafiki kwa kukubali tu mwaliko wa mutu. Lakini, ile ni urafiki tu ya jina. Juu ku Enternete watu wako na uwezo wa kupanga maneno ya kusema, na kwa kiasi fulani wanajua namna ya kupambana na mawazo yenye watu wanaweza kuwa nayo juu yao, ni mwepesi kuficha vile wako kabisa. Kwa hiyo, ni jambo ya maana kufikiri kwa uangalifu ni watu wa namna gani njo utakubali kuwa marafiki wao. Usiogope kukatala mwaliko wa kuwa rafiki ya mutu fulani mwenye haujue kabisa hata kama ile inaweza kumuumiza. Juu ya hatari zenye zinaweza kutokea, watu fulani washakaamua kutotumia site yoyote ya Enternete ya kupashana habari. Lakini, kama unachagua kutumia site ya Enternete ya kupashana habari, ni mambo gani unapaswa kufikiria?
MUANGALIE VIDEO TUMIA KWA HEKIMA SITE ZA ENTERNETE ZA KUPASHANA HABARI, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Unapaswa kufikiria nini mbele ya kuweka ku Enternete maelezo ao picha fulani?
Juu ya nini unapaswa kuchagua kwa uangalifu marafiki wako wa ku Enternete?
Juu ya nini unapaswa kujiwekea mipaka kuhusu wakati yenye unapitisha ku site ya Enternete ya kupashana habari?—Efe 5:15, 16