UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 9-11
Mufano wa Muzeituni
Sehemu mbalimbali za muzeituni wa mufano zinafananisha nini?
Muti unafananisha kutimizwa kwa mambo yenye Mungu alipenda kufanya kupitia agano lake na Abrahamu
Shina ni Yesu, yeye njo sehemu ya kwanza ya uzao wa Abrahamu
Matawi ni wale wote wenye kufanyiza sehemu ya pili ya uzao wa Abrahamu
Matawi yenye “yalikatwa” ni Wayahudi wa asili ao wa kizalikio wenye walikatala Yesu
Matawi yenye ‘yalipandikizwa’ ni Wakristo wenye walitiwa mafuta na roho wenye walitoka mu mataifa ingine
Vile Biblia ilitabiri, uzao wa Abrahamu, ni kusema Yesu na wale 144 000, wataletea “watu wa mataifa” baraka.—Ro 11:12; Mwa 22:18
Namna Yehova alitimiza kusudi lake kuhusu uzao wa Abrahamu inanifundisha nini?