Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Mwezi wa 6 uku. 8
  • Ufanye Nini Juu Funzo Yako ya Pekee Ikuletee Faida Zaidi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufanye Nini Juu Funzo Yako ya Pekee Ikuletee Faida Zaidi?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tusitawishe Urafiki wa Karibu Pamoja na Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kufanya Wakati wa Funzo Uwe Wenye Kufurahisha Zaidi na Wenye Faida Zaidi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Nini Njo Inaweza Kukusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
mwb19 Mwezi wa 6 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Ufanye Nini Juu Funzo Yako ya Pekee Ikuletee Faida Zaidi?

SABABU GANI NI LAZIMA: Kujifunza kipekee neno la Mungu kunatusaidia “kabisa kuelewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini” wa kweli ya Biblia. (Efe 3:18) Kunatusaidia pia kuendelea kuwa bila lawama na bila kasoro katikati ya watu wenye wanajiendesha mubaya na kuendelea “kushika sana neno la uzima.” (Flp 2:15, 16) Funzo ya pekee inatupatia nafasi ya kuchagua habari yenye tunaona kama itatusaidia kipekee. Unaweza kufanya nini juu funzo yako ya pekee ikuletee faida zaidi?

NAMNA YA KUFANYA:

  • Tia alama chini ya maandiko na uandike maelezo fulani mu Biblia yako ya funzo, ikuwe unatumia Biblia ya karatasi ao ya kielektroniki

  • Wakati uko unasoma Neno la Mungu, jiulize hii maulizo: ‘Nani? Nini? Wakati gani? Wapi? Juu ya nini? Namna gani?’

  • Tafuta habari zaidi. Tumia vyombo vya kutusaidia kutafuta habari vyenye tuko navyo ili kutafuta habari juu ya wazo fulani ao andiko fulani

  • Fikiri sana juu ya mambo unasoma ili uone namna ya kuitumikisha mu maisha yako

  • Tumikisha mambo yenye unajifunza mu maisha yako ya kila siku.​—Lu 6:47, 48

MUANGALIE VIDEO FUNZO YA PEKEE YA MUZURI INATUSAIDIA TUKUWE NGUVU KIROHO, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Wengine wanasema nini juu ya funzo ya pekee?

  • Juu ya nini tunapaswa kuanza kila funzo ya pekee na sala?

  • Ni nini inaweza kutusaidia kuelewa muzuri andiko fulani?

  • Ni alama gani tunaweza kutia mu Biblia yetu ya funzo?

  • Juu ya nini inaomba kufikiri sana wakati tunajifunza Neno la Mungu?

  • Tunapaswa kufanya nini na mambo yenye tunajifunza?

Dada anachimba sana wakati wa funzo yake ya pekee ya Biblia; ndugu anatia alama za rangi mbalimbali mu Biblia yake; dada anazungumuza na wanaume wawili kuhusu maelezo yenye aliandika mu Biblia yake; ndugu anasali

“Ninapenda sana sheria yako! Ninafikiri sana juu yake muchana wote.”​—Zb 119:97

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine