MAISHA YA MUKRISTO
Ujikaze Kujua Muzuri Namna Mambo Ilikuwa
Wakati uko unasoma habari zenye kuwa mu Biblia, ujikaze kujua muzuri namna mambo ilikuwa. Ujifunze habari yenye kutangulia na yenye kufuata habari yenye uko unasoma, watu wenye kuzungumuziwa, na sababu zenye pengine ziliwachochea watende katika njia fulani. Tumia uwezo wako wa kuona mambo katika akili ili kuona mahali mbalimbali, kusikia sauti mbalimbali, harufu mbalimbali, na kujisikia namna watu wenye kuzungumuziwa walijisikia.
MUANGALIE VIDEO FANYA USOMAJI WAKO WA BIBLIA UKUWE MUZURI ZAIDI—SEHEMU, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Pengine ni sababu gani zilifanya ndugu za Yosefu wasipatane naye sikuzote?
Pengine ni juu ya nini wakati fulani ndugu za Yosefu walitenda kwa ukali na bila kufikiria matokeo?
Tunaweza kujifunza nini katika Biblia juu ya Yakobo, baba ya Yosefu?
Yakobo aliachia watoto wake mufano gani muzuri juu ya namna ya kuelewana na wengine?
Kuangalia hii video kumekuletea faida gani?