UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 6-7
“Sasa Utaona Mambo Yenye Nitamutendea Farao”
Mbele alete mapigo katika inchi ya Misri na kukomboa Waisraeli kutoka katika utumwa, Yehova aliambia Waisraeli mambo yenye alikuwa karibu kufanya. Wangeona namna Yehova angeonyesha nguvu yake katika njia yenye walikuwa hawajaonaka, na kwa kweli, Wamisri wangejua kama Yehova njo Mungu wa kweli. Wakati ahadi za Mungu zilitimia, ile ilitia nguvu imani ya Waisraeli, na ilisaidia kumaliza uvutano wa dini za uongo zenye zilikuwa Misri.
Namna gani hii habari ya Biblia inakuhakikishia zaidi kama ahadi za Yehova juu ya wakati wenye kuja zitatimia?